Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi.

WAHAMIAJI haramu 56, Raia wa nchini Ethiopia, wamekamatwa katika Kijiji cha Jiungeni, Kata ya Ruvu, wilaya ya Same, Mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Ofisini Kwake, Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Robert Boaz alisema Wahabeshi hao walikamatwa majira ya saa sita usiku, usiku wa kuamkia Juzi, wakiwa katika Lori aina ya Fuso, yenye namba za usajili, T188 AYU, mali ya kampuni ya E.Lyimo ya Mjini Moshi.

Kamanda Boaz alisema baada ya kupata taarifa ya uwepo wa watu wanaotiliwa mashaka kijijini hapo, polisi walianza kufuatilia na kuwahi Gari hilo likiwa na Wahamiaji hao ambao hata hivyo bado haijafahamika walikuwa wakielekea wapi.

“Polisi waliwahi baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi na kukamata wahabeshi 56, walikuwa wanasafirishwa kwenye Lori aina ya Fuso, namba za usajili T188 AYU mali ya E.Lyimo ya mjini Moshi, bado hatujafahamu walikuwa wanaelekea wapi lakini uchunguzi unaendelea,” alisema Boaz.

Kamanda Boaz alisema mbali na Wahabeshi hao 56, Polisi walifanikiwa kuwakamata Watanzania Watatu akiwemo Dereva wa Lori hilo, aliyetambulika kwa jina la Daniel Mfinanga pamoja na wenzake wawili ambao majina yao yanahifadhiwa kutokana na sababu za kiupelelezi.

Aidha Kamanda Boaz aliongeza kuwa Utingo wa Lori hilo, aliyemtaja kwa jina la Ismael Juma, alifanikiwa kutoroka na kwamba jeshi hilo kwa sasa linaendelea na msako ili kumtia mbaroni.
Kundi la wahamiaji haramu zaidi ya 40 wanaodhaniwa kuwa ni wa kutoka Ethiopia na Somalia wakishuka kwenye Lori aina ya fuso katika kituo kikuu cha muda baada ya kukamatwa wilayani Same wakijiandaa kusafirishwa kwenda nchi ya Afrika kusini.
Wahamiaji haramu wakiwa katika ofisi za kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro muda mfupi baada ya kufikishwa wakitokea wilayani Same ambako walikutwa wakijiandaa kutaka kusafirishwa kwenda Afrika kusini.
Gari aina ya Fuso lililokutwa likiwa limebeba wahamiaji haramu tayari kuwasafirisha kwenda Afrika kusini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Miaka ya 70 na 80 Wabongo walitumia njia hiyo hiyo kuelekea Ugiriki. Sasa hivi TZ watu wametajirika ndio wakisafiri wanaenda kwa ndege. Wengi walilizwa Bongo na ndugu zao kwa kuuzwa nyumba, viwanja, na vyombo vya dhahabu ili kugharamia nauli ya kwendea Ulaya.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...