Na Denis
Mlowe.Aliyekuwa Arusha
WANANCHI wa wanaozunguka hifadhi
ya Taifa ya Ziwa Manyara iliyoko mkoani Arusha wametakiwa kulinda hifadhi
hiyo kwa kuachana na kulima katika vyanzo vya maji na maeneo yanayoizunguka
hifadhi hiyo.
Wito huo
umetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa TANAPA Dk.Ezekiel Dembe hivi karibuni wakati
akizungumza na wanahabari mkoa wa Iringa ambao walikuwa katika ziara
ya mafunzo ya kutangaza utalii katika Hifadhi za Kaskazini.
Alisema kuna hatari kubwa ya Ziwa Manyara kukauka zaidi kutokana na wananchi kuendelea kulima na kupelekea ziwa kujaa tope kutokana na kilimo hicho cha pembezoni.
Alisema kuna hatari kubwa ya Ziwa Manyara kukauka zaidi kutokana na wananchi kuendelea kulima na kupelekea ziwa kujaa tope kutokana na kilimo hicho cha pembezoni.
Dk.Dembe
alisema kutokana na kisichozingatia uhifadhi wa Ziwa Manyara baadhi ya ofisi za
hifadhi hiyo zimeharibika vibaya kutokana na mafuliko hivyo Tanapa wana mpango
wa kutafuta eneo jingine ili kujenga ofisi hizo.
Akizungumzia ubovu wa miundo mbinu katika hifadhi za Taifa alisema kuwa TANAPA wapo katika mkakati kuboresha miundo mbinu hiyo ili kuvutia zaidi watalii wanaofika katika hifadhi hizo kuendelea kupitika kwa urahisi kwa mwaka
Akizungumzia ubovu wa miundo mbinu katika hifadhi za Taifa alisema kuwa TANAPA wapo katika mkakati kuboresha miundo mbinu hiyo ili kuvutia zaidi watalii wanaofika katika hifadhi hizo kuendelea kupitika kwa urahisi kwa mwaka
Akielezea kuhusu hifadhi ya Taifa Ruaha iliyoko Iringa kutangazwa kama ilivyo hifadhi za Kaskazini Dk. Dembe, alisema kuwa hivi sasa mkakati umewekwa wa kuelekeza nguvu ya kuitangaza hifadhi hiyo ili kuvutia watalii zaidi japo alisema changamoto kubwa ni upatikanaji wa mafuta ya Ndege ambazo zinaleta watalii ambao hulazimika kujaza mafuta Dodoma .
“Hata hivyotumeanza mkakati wa kuhakikisha hifadhi ya Katavi na Ruaha katika viwanja wa ndege vilivyopo huko kunakuwa na mafuta ya ndege kupunguza gharama ambazo watalii wanatumia kwa sasa” alisema Dk. Dembe
Alisema TANAPA wako katika mchakato wa kutafuta wawekezaji wa kujenga Hotel za kisasa katika hifadhi ya Ruaha ili kuvutia watalii wengi zaidi.
Kuhusu usalama wa watalii alisema kuwa TANAPA wamejipanga kuweka usalama mzuri wa watalii ili ni pamoja na kuanzisha ulinzi wa askari watakaofanya kazi ya kulinda watalii pekee.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...