Rais wa taasisi ya isiyo ya kiserikali ya ISACA Tanzania, Boniface Kanemba akifungua semina hiyo.
Wadau.
Mshiriki wa semina hiyo akiuliza swali.
Washiriki wa semina.
Baadhi ya washiriki wa semina hiyo.
Ofisa wa PPF akitoa mada.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa wakala wa Serikali Mtandao ambaye pia ni Makamu wa Rais wa taasisi ya isiyo ya kiserikali ya ISACA Tanzania, Dk. Jabir Bakari Kuwe (kulia), akitoa mada wakati wa mkutano wa wadau, kuhusu usalama wa fedha kwenye mitandao ya simu pamoja na mkutano mkuu wa taasisi hiyo uliofanyika Dar es Salaam.
Dk. Carina Wangwe akitoa mada.
Rais wa taasisi ya isiyo ya kiserikali ya ISACA Tanzania, Boniface Kanemba (kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano wa wadau, kuhusu usalama wa fedha kwenye mitandao ya simu pamoja na mkutano m.kuu wa taasisi hiyo uliofanyika Dar es Salaam.
Mmoja wa washiriki wa semina hiyo akitoa mada.
Rais wa taasisi ya isiyo ya kiserikali ya ISACA Tanzania, Boniface Kanemba akizungumza na waandishi wa habari.
--------------------------------
--------------------------------
WANANCHI wametakiwa kuepuka kugawa taarifa zao muhimu kuhusiana
na mawasiliano yao ya simu pamoja na taarifa muhimu za kibenki.
Tahadhari hiyo imetolewa kufuatia ongezeko la wizi wa fedha
katika akaunti za benki na simu za mkononi unaofanywa na matapeli hapa nchini.
Rais wa Taasisi inayojishugulisha na Ukaguzi wa Mitandao ya
ISACA Tanzania , Boniface Kanemba alisema kuwa matapeli hao wanaweza
kutumia nambari za simu za mkononi na akaunti ya benki kujua namba za siri za
kuchukulia fedha.
Alisema kuwa ili kuepuka wizi wa aina hiyo ni vema wananchi
wakachukua tahadhari dhidi ya utoaji wa taarifa kwa kuwa inakuw ani vigumu
kuwakamata pindi wakishafanya uhalifu huo.
Alisema kuwa matapeli wa aina hiyo walikuwa zaidi katika Kenya
na lakini kwa sasa inaonekana wamevamia zaidi hapa nchini na kutumia ujuzi huo.
Alisema kuwa kwa ukanda wa Afrika Mashariki peke yake kiasi cha
zaidi ya trilioni 80 zimeibwa kwa njia ya utapeli.
Aliongeza kuwa ili kukabiliana na hali hiyo tayari taasisi yake
inaendelea na utoaji wa semina mbalimbali kwa wadau wa teknolojia ya
mawasiliano na watu wa usalama kwa ujumla.
"Najau wizi wa aina hii ulikuwa zaidi katika nchi za Ulaya
na Afrika Magharibi na ukanda huu wa Afrika ya Mashariki ulikuwa zaidi Kenya
lakini kwa sasa hawa matapeli wamevamia ukanda huu wa Afrika Mashariki na hali
inazidi kuwa mbaya"alisema Kanemba.
Taasisi hiyo ya ISACA ilianza kazi hapa nchini mwaka 2003 na
imekuwa ikifanya ukaguzi wa usalama wa fedha na matukio mengine muhimu kwa njia
ya mtandao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...