Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Bashir Mrindoko akieleza namna anavyo
kasirishwa na mwenendo wa kusuasua kwa baadhi ya miradi ya maji nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Kigoma,
ASaimon Lupuga aliyesimama nyuma akijibu swali la Katibu Mkuu namna wakandarasi
wanavyotekeleza miradi ya maji mjini Kigoma, wengine ni baadhi ya maafisa wa Wizara,
wakuu wa mamlaka za maji, wakandarasi na wakandarasi washauri.
Na Athumani Shariff,
Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Bashir Mrindoko amelazimika kukutana na
wakandarasi na wakandarasi washauri wanaotekeleza baadhi ya miradi ya maji nchi nzima
Ubungo Maji Makao Makuu ya Wizara ya Maji jijini Dar es Salaam.
Kikao hicho pia kiliwahusisha wakurugenzi wote wa Wizara ya Maji, kilikuwa na lengo
lakutathini mwenendo wa miradi ya maji nchini na kuangalia namna ya kuharakisha
utekelezaji wa miradi hiyo.
Katika kikao hicho Katibu Mkuu hakufurahishwa na namna ambavyo wakandarasi wengi
wanavyofanya kazi polepole huku wananchi wakiendelea kuteseka kwa kero ya kukosa
huduma ya maji.
“Si ridhiki na namna munavyofanya kazi haswa wakandarasi wa miradi ya Morogoro, nataka
muangalie namana ambavyo munaweza kufanya ili mukamilishe miradi hiyo kwa wakati”
alisisitiza Mrindoko.
Aidha alisema hatosita kukatisha mikataba na wakandarasi wazembe na wale ambao
wanachelewesha miradi kwa visingizio visivyo vya msingi.
“Hapa juzi tu nimekatisha mkataba na mkandarasi wa mradi wa maji wa Chalinze, hivyo kwa
yoyote atakayezembea sitoacha kumkatishia mkataba, na atake haribu kazi nitamshitaki
katika bodi ya wakandarasi ambayo na mimi mwenyewe ni mjumbe” aliongezea Katibu
Mkuu.
Baada ya maelezo yake mafupi, Katibu Mkuu aliwasimamisha wakandarasi washauri katika
kila mradi kueleza namna miradi wanayoisimamia inavyotekelezwa na kisha kuwanyanyua
wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo kueleza jinsi wanavyotekeleza na kuweka ahadi lini
wataikamilisha.
Wakieleza katika kikao hicho, baadhi ya wakandarasi wamejitetea kuwa miradi mingi ya
maji imekuwa ikichelewa kutokana na changamoto mbalimbali, vikiwemo ukosefu wa vifaa
vya kutendea kazi, malighafi, ucheweshwaji wa bidhaa bandarini, ukosefu wa umeme wa
uhakika, taratibu za TRA na upatikanaji wa mabomba viwandani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...