Mara baada ya kusaini mkataba huo wa kucheza raundi 10 za ubingwa wa Taifa Kg 60 amesema atafanya mazoezi ya kutosha kuhakikisha ana msambaratisha mpinzani wake raundi za awali kwa kuwa alikuwa anachonga sana juu yake.
Mpambano huo unaodhaminiwa na Promota Maarufu nchini Jay Msangi utakuwa na msisimko wa aina yake kutokana na mabondia hawo kuwa gumzo katika ulimwengu wa masumbwi ndani na nje ya nchi.
King Class aliongeza kwa kusema;"Nipo fiti, nimejiandaa na ninasubiri tu kuvishwa ubingwa huo wa Taifa kwani Cheka hana ujanja kwangu mbinu zake zote nimesha zikamata".
King Class Mawe ananolewa na jopo la makocha wanao ongozwa na Habibu Kinyogoli 'Masta' Rajabu Mhamila 'Super D' na Kondo Nasoro.
Bondio huyo amewashukuru wadau wa mchezo wa ngumi kwa kumuwezesha kuchaguliwa kuwa bondia bora wa mwaka katika uzito wake na kuwapita mabondia wengine wanne na yeye kuibuka kidedea katika kin'yan'gan'yiro hicho
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...