Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, amefika katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam kuwajuilia hali Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma Mhe. Haroun Ali Suleiman, pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu Mzee Cleopa David Msuya waliolazwa katika hospitali hiyo. 
Viongozi  hao wamelazwa katika hospitali hiyo wakisumbuliwa na matatizo ya moyo. Wakizungumza na Makamu wa Kwanza wa Rais, wamesema wanaendelea vizuri na kwamba afya zao zinaendelea kuimarika siku hadi siku, tofauti na walipofikishwa hospitalini hapo. 
Waziri Haroun anatarajiwa kupelekwa nchi Afrika ya Kusini kwa uchunguzi na matibabu zaidi. Kwa upande wake Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, amewaombea viongozi hao wapone haraka ili waendelee na majukumu ya kulitumikia taifa.
  Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akimjuilia hali Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma Mhe. Haroun Ali Suleiman katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akimuombea dua  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi na Utumishi wa Umma Mhe. Haroun Ali Suleiman, alipokwenda kumjulia hali katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akimjuilia hali Waziri Mkuu mstaafu Mzee Cleopa David Msuya katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akimjuilia hali Waziri Mkuu mstaafu Mzee Cleopa David Msuya katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Picha na Salmin Said, OMKR

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Oooh huyu Rais anasafjri saana, mngeoata wapi hospitali nzuri kama hii. . . Hapa hawa tayari wangekua wamepelekwa India

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...