Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi Bw. Morice Oyuke kutoka Ofisi ya
Taifa ya Takwimu (katikati) akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu ukuaji wa Pato la
Taifa kwa robo mwaka ya tatu ya mwaka 2013 ambapo katika kipindi cha Julai – Septemba,
2013 Pato la Taifa kwa bei za soko liliongezeka kwa kasi ya asilimia 6.5 ikilinganishwa na
asilimia 7.2 kwa kipindi kama hicho mwaka 2012. Kulia kwake ni Bw. Juma Omary, Mchumi
Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Tume ya Mipango na kushoto ni Bw. Daniel Masolwa Meneja
Takwimu za Pato la Taifa kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Takwimu za
Uchumi Bw. Morice Oyuke kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (katikati) akizungumza kuhusu
ukuaji wa Pato la Taifa kwa robo mwaka ya tatu ya mwaka 2013 katika ukumbi uliopo Ofisi ya
Rais Tume ya Mipango, Dar es Salaam. (Picha na Veronica Kazimoto).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...