Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mwl. Julius Nyerere
(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wapiga picha maarufu toka
vyombo mbalImbali vya habari hapa nchini (enzi hizo) wakati alipokuwa akiwaaga ikulu jijini Dar es Salaam mwaka 1985.
Toka kushoto waliosimama ni mpiga picha Mkuu wa Gazeti la Mfanyakazi
Maxi Madebe, Mpiga picha mkuu wa SHIHATA Sam Mmbando, Mpiga picha mkuu
wa gazeti la Daily News Vicent Urio na mpiga picha mkuu wa serikali
John Baptist Makwaia.
Wengine ni mpiga picha wa sinema wa taasisi ya vielelezo (AVI),Sailen,
wapiga picha wa SHIHATA Juma Dihule na Adinan Mihanji. Mwisho ni mpiga
picha wa maelezo, Moshy Kiyungi.
Waliochuchumaa wa pili toka kushoto ni mpiga picha wa maelezo, Charles
Kagonji, mpiga picha Daily News Gervas Msillo na mpiga picha wa
maelezo Mwanakombo Jumaa. wengine ni mpiga picha mkuu wa Uhuru na
Mzalendo, Khatib Ally na mpiga picha wa maelezo Raphael Hokororo.
Home
Unlabelled
TASWIRA YA WAPAMBANAJI WA ENZI ZA MWALIMU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...