Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Ngumi za Kulipwa la Afrika ya Mashariki na Kati (ECAPBA) katika kikao
chake kilichokaa tarehe January 4, 2014 jijini Kigali, Rwanda, limefanya mabadiliko ya kujaza nafasi za
uongozi.
Yassin Abdalla (Ustaadh) wa Tanzania ameteuliwa kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa ECAPBA. Abdalla
ambaye ni Rais wa TPBO amejaza nafasi ya Celestino Mindra wa Uganda aliyekuwa Rais wa Baraza la Ngumi
la Jumuiya ya Madola na Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa ya Uganda (UPBC)
Simon Kategole wa Uganda, ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa ECAPBA kujaza nafasi iliyoachwa wazi na
Shaban Ogolla wa Kenya ambaye yuko masomoni nchini Marekani. Daudi Chikwanje wa Malawi anachukua
nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa ECAPBA.Aidha, Nelson Sapi wa Zambia ameteuliwa kuwaNaibu Mweka
Hazina wa ECAPBA akimsaidia Nemes Kavishe wa Tanzania.
Bonifawa Wambura wa Tanzania anabaki kuwa Afisa Habari wa ECAPBA wakati wajumbe wanne
wameongezwa kwenye Kamati ya Utendajji kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Malawi na Ethiopia
pamoja na Roman Chuwa wa jiji la Arusha.
Aidha, ECAPBF inamshukuru Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Gaudence Lyimo kwa kukubali kuwa mlezi wake
na kuipatia ofisi katika Manispaa ya jiji la Arusha ikikumbukwa kwamba ndicho chombo cha kuwaunganisha
vijana cha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Katika malengo yake, ECAPBA itafanya kazi kwa karibu sana na
Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) ili iweze kuwa chachu ya utekelezaji wa maamuzi ya Jumuiya katika
ukanda wa Afrika ya Mashariki na Kati.
Kwa kutambua kuwa, Jumuiya ya Afrika ya Mashariku ni chombio cha uchumi cha kuunganisha nguvu za
watu wa Afrika ya Mashariki, ECAPBA imedhamiria kuyafanyia utekelezaji maamuzi yote yanayohusu
maendeleo ya vijana pamoja na ushirikiano wa utamaduni na michezo wa EAC. Aidha, ECAPBA imedhamiria
kuleta chachu katika kujenga nguvu na kutengeneza ajira kwa vijana wa Afrika ya Mashariki na Kati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...