Na Bin Zubeiry

AZAM FC imerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kufuatia ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Ashanti United jioni hii Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Ushindi huo unaifanya timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake ifikishe pointi 40 baada ya kucheza mechi 18, ikiishusha nafasi ya pili, Yanga SC yenye pointi 38 ingawa ina mechi moja mkononi.
Gaudence Exavery Mwaikimba alifunga kila kipindi dhidi ya timu yake ya zamani, mabao yote akimalizia kazi nzuri ya mshambuliaji Mganda, Brian Umony.


Beki Aggrey Ambroce Morris alifunga kwa penalti bao la kwanza la Azam baada ya kipa wa Ashanti United, Juma Mpongo kumchezea rafu Umony na Mwaikimba akafunga la pili akimalizia krosi ya Mganda huyo pia.
Beki Said Morad ‘Mweda’ aliiadhibu pia timu yake ya zamani kipindi cha pili akiunganisha kona iliyochongwa na Khamis Mcha ‘Vialli’ kabla ya Mwaikimba kuhitimisha karamu ya mabao ya Azam kwa bao safi la nne akiuwahi mpira uliotemwa na kipa Mpongo baada ya shuti la Umony.
Ikumbukwe Mwaikimba alipangwa leo kwa sababu washambuliaji chaguo la kwanza la kocha Joseph Marius Omog, John Bocco ni majeruhi na Kipre Tchetche alikuwa anatumikia adhabu ya kadi nyekundu.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...