Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiangalia vifaa mbali mbali katika chuo cha mafunzo ya Amali  kichofundisha wanawake pekee kutoka nchi mbali mbali Duniani ikiwemo Zanzibar,katika cha  Tilonia,Wilaya ya  Ajmer Jimbo la Rajastan akiwa  katika siku ya pili ya ziara yake Nchni India pamoja na Ujumbe aliofuatana nao
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipokea zawadi mara alipowasili katika Chuo cha Mafunzo ya Amali kiitwacho Tilonia,Wilaya ya  Ajmer  Jimbo la Rajastan akiwa  katika siku ya pili ya ziara yake Nchni India pamoja na Ujumbe aliofuatana nao

 Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maliasili Affani Othman Maalim (kulia) kwa niaba ta Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akitiliana saini makubaliano  ya Uanzishwaji wa Chuo cha Mafunzo ya Amali kwa Wanawake na Chuo cha Barefoot cha India ambapo muanzilishi wa Chuo hicho Bw.Bunker Roy alitia saini (kulia) saini hiyo ilifanyika wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwa katika ziara rasmi Nchini India na ujumbe wake.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akibadilishana mawazo na Bw.Bunker Roy Muanzilishi wa Chuo cha Mafunzo ya Amali kwa Wanawake katika Kijiji cha Tilonia  Wilaya ya Ajmer Jimbo la Rajastan pamoja na Balozi wa India Nchini Tanzania  Debnath Shaw (kulia) baada ya Saini ya makubaliano ya uannzishwaji wa Chuo kama hicho Zanzibar. 
Picha ya pamoja baada ya ziara hiyo. Picha zote na Ramadhan Othamn,Ikulu Zanzibar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...