Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Lindi(LPC) Inatoa Pongezi kwa ACP Renatha Mzinga(pichani) aliekuwa Ofisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi kwa kuteuliwa na MKUU wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa LINDI.
Taarifa iliyotolewa leo na Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Lindi,Abdulaziz Ahmeid ameeleza kuwa kuwa Klabu hiyo Imepokea mabadiliko hayo na kuhaidi Ushirikiano mkubwa baina ya klabu na Jeshi hilo.
 "Kwa niaba ya wanahabari nampongeza Mkuu wa Jeshi hilo IGP Mangu kwa uteuzi huu nasi tutamuunga mkono katika kazi zetu za kila siku kwa kuwa kwa kipindi kifupi alichokuwapo Lindi Tumeona Ushirikiano wake kwa wanahabari kwa kujadiliana na kuwa huru kutoa habari Isitoshe tumeshuhudia alivyoweza kuwaunganisha Polisi na kujua baadhi ya Changamoto zao hususan Alivyowaunganisha askari wa kike(WP) Katika kuunda mtandao wa polisi wanawake hali iliyoonekana ni mabadiliko makubwa' 
Hivi karibuni Kamanda Renatha alifanikisha zoezi la Usafi na kutoa misaada kwa kituo cha walemavu kilichopo Manispaa ya Lindi na askari hao kushiriki kutoa walichonacho kusaidia walemavu hao 
Waandishi wa habari hufanya kazi kwa karibu na jeshi hilo hivyo tunatarajia kupata Ushirikiano mkubwa toka kwa Kamanda Mzinga na wasaidizi wake wakati wa matukio ya dharura na yasiyo ya dharura na kuondoa hali ya Polisi wachache kuona Waandishi wa Habari ni maadui wakubwa kutokana na maovu yao.
 Mwaka jana Klabu ya waandishi wa habari ilifanya kazi vizuri na Jeshi hilo, ilimalizia taarifaa ya  LPC Iliyotolewa na Mwenyekiti wake Abdulaziz Ahmeid ambae pia ni mwandishi wa Channel ten mkoa wa Lindi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...