Katibu Tawala Mkoa wa Katavi akimwongoza Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto,Mama Anna Maembe wakati akikagua eneo la chuo cha maendeleo Msaginya wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani humo anaye mfuatia kushoto kwa Katibu Mkuu ni Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya Nsimbo Alex Magesa Na Mwisho mwenye SUTI YA kijivu ni Mkuu wa Chuo Msaginya Peter Kikunda ambaye ni mwenyeji akiwatembeza wageni.
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto,Mama Anne Maembe akipatiwa maelezo kuhusu bweni la wananchi wa kike liliezuliwa na upepo kufuatia mvua mwaka jana hali iliyofanya kusimama kwa masomo katika chuo hicho kutokana na ukosefu wa mahali pa kulala kwa wanafunzi wa Kike.
Baadhi ya majengo ya chuo Msaginya yanaonekana kuchaka kutokana na kukosa ukarabati kwa muda mrefu hali inayoonesha chuo kama vile kimesahaulika ambacho kinamilikiwa na wizara ya maendeleo ya jamii,lakini ni mali ya wananchi ingawa hawaoni umuhimu wa kuwa na chuo hicho,juhudi za makusudi zinahitajika na ubunifu zaidi ili kunusuru chuo hicho.
Na Kibada Ernest- Katavi.
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto,Anna Maembe ameshauri watendaji wa Wizara hiyo kuwa wabunifu katika utendaji wao wa kazi za kila siku kwenye maeneo yao ili kuleta mabadiliko katika jamii wanayoitumikia katika utendaji wao wa kazi.
Katibu Mkuu alitoa kauli hiyo mkoani Katavi alipokutembelea mkoa huo na kukutana na watendaji wa Wizara yake na kupata nafasi ya kukitembelea Chuo cha Maendeleo ya wananchi Msaginya kilichoko Halmashauri ya Nsimbo Wilayani Mlele ambacho kinakabiliwa na changamoto kibao hali iliyosababisha kushindwa kusajiri wanachuo wa kujiunga katika fani mbalmbali mwaka huu wa masomo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...