Mwenyekiti wa Shirika la Afya na Elimu (MMHEN) liliyopo Mikocheni, Regent Estate, Dar es Salaam, anapenda kuutangazia umma kuwa tarehe 06/02/2014 kuanzia saa 02:00 asubuhi Shirika, pamoja na Taasisi zake zikijumuisha Kairuki Hospital (KH), Hubert Kairuki Memorial University (HKMU) na Mikocheni School of Nursing (MSN) wataadhimisha miaka 15 ya kutokwa na muasisi wa MMHEN na Taasisi zake PROF. HUBERT CLEMENCE MWOMBEKI KAIRUKI .

Katika kuadhimisha siku hiyo, MMHEN na taasisi zake zilizo chini ya zitatoa huduma ya afya bila malipo kwa jamii pamoja na uchangiaji wa damu kwa hiari kwa ushirikiano wa BLOODAT na DAMU SALAMA itakayotolewa katika viwanja vya shule ya msingi Mikocheni kwa muda wa siku mbili (2) kuanzia tarehe 05/01/2014 hadi 06/02/2014. Shughuli hizi zitafuatiwa na mada (public lecture) itakayotolewa na Dr. Kaushik Ramahiya kutoka Hindu Mandal Hospital kuanzia saa 8:30 mchana ukumbi wa mihadhara , ghorofa ya tano hapo HKMU.

Pamoja na kutoa huduma ya afya bila malipo, Mwenyekiti wa MMHEN pia atakabidhi jengo la madarasa manne (4), ambalo limekarabatiwa na Kairuki Hospitali, vifaa kwa ajili ya matumizi ya ofisi ya shule pamoja na msaada kwa wahanga wa maafa ya mafuriko yaliyotokea Dumila mkoani Morogoro, hivi karibuni.

Kwa taarifa zaidi, wasiliana na : Gerlad Manongi manongiss@yahoo.co.uk 0715 847 444 or 2700021-4 : Arafa Juba 0715 289 264 arafamody@yahoo.com E-mail : info@kairukihospital.org Website: www.kairukihospital.org

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...