Na Abdulaziz Video,lindi 
Kampeni za Uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kiwalala umefungwa na Mgeni Rasmi Mbunge wa Jimbo la Mtama, Mhe. Bernard Membe kwa kuwataka wananchi wa kata hiyo kutofanya makosa kwa kumchagua ndg Zahoro Shineni 
Mkutano huo ambao ulihudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Chama mkoa wa Lindi akiwemo katibu mkuu wa Umoja wa Vijana Taifa pamoja na Viongozi wa CCM wa mkoa wa Mtwara waliokuwa wakielekea katika kufunga kampeni za Uchaguzi Mdogo Huko Mkwiti Mkoani Mtwara

Mbunge wa Jimbo la Mtama ambae pia ni Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe akimnadi Mgombea wa Udiwani wa kata ya kiwalala kupitia CCM, Zahoro Shineni Hamis katika mkutano wa kufunga Kampeni uliofanyika katika kijiji cha Mahumbuka Lindi Vijijini

Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM Taifa,Sixtus Mapunda akiwaasa Wananchi wa Kiwalala kumchagua Mgombea wa CCM katika Uchaguzi mdogo wa Udiwani kata ya Kiwalala
Moja ya Burdani zilizotolewa na wasanii katika kufungwa kwa kampeni za CCM
Mbunge wa Jimbo la Kilwa kaskazini, Mhe. Murtaza Mangungu akimuombea kura mgombea wa Udiwani katika kijiji cha kiwalala

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...