Wagombea nao wakijifariji kwa makofi ya wajumbe
KAIMU Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga amewasihi wajumbe wa mkutano huo kumchangua mgombea anayoonekana kukubalika kwa asilimia 60 kwa wapiga kura.
"Falsafa ya chama kwanza, mtu baadaye lazima tuipime vizuri, tunahitaji ushindi na ili tupate ushindi lazima tuangalie wananchi wanataka nini," alisema.
Akifungua mkutano huo, Mtenga aliwataka wagombea ndani ya chama hicho wawe na utamaduni wa kukubali matokeo kwa afya ya chama.
Alisema wagombea wote tisa waliojitokeza katika kura hizo za maoni wana sifa za kuwa wabunge na akawataka wajumbe kutumia busara zaidi wakati wakifanya uamuzi.
Alisema mchakato wa kura za maoni ndani ya chama hicho umecchukua siku mbili hali itakayosaidia kukinusuru chama na mipasuko.
“Tulikuwa na kawaida ya kufanya kura za maoni kwa zaidi ya mwezi mmoja; hali hiyo ilikuwa ikiwaacha wagombea katika majeraha makubwa ya matumizi ya fedha,” alisema.
Alisema majeraha hayo yamekuwa yakichangia hasira kwa wagombea walioshindwa ambao badala ya kukisaidia chama kipate ushindi, hufurahia kinapopoteza nafasi.
Alisema kwa mtaji walionao, CCM wana hakika na ushindi wa kishindo katika jimbo hilo lililoachwa wazi na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa.
Waliojitokeza kupitia katika chama hicho ni pamoja na Jackson Kiswaga, Hafsa Mtasiwa, Godfrey Mgimwa.
Wengine ni Gabriel Kalinga, Peter Mtisi, Edward Mtakimo, Bryson Kisaba, Msafiri Pagamila na Thomas Mwakoka.
|
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...