Mkuu wa mkoa wa Lindi na ujumbe wake wakikagua Zahanati ya Kijiji cha Kikulyungu wilayani Liwale
 Nyumba ya wahudumu wa Afya kijiji cha kikyulungu inayojengwa kwa Msaada wa Benjamin  Mkapa Foundation
  Mkuu wa mkoa wa Lindi Mhe. Ludovick Mwananzila (mwenye suti ya kijivu) akikagua miradi ya Maendeleo wilayani Liwale
 Mkuu wa mkoa wa lindi MheLudovick Mwananzila akihutubia wananchi wilayani liwale  kulia ni mkuu wa wilaya ya Liwale Mhe.  Ephraim Mmbaga
Mkuu wa mkoa wa Lindi akikagua ujenzi wa maabara shule ya sekondari Nicodemus Banduka wilyani Liwale. Picha na habari na Abdulaziz Video.
-----------------------------------------
 Mkuu wa mkoa wa Lindi Mhe. Ludovick Mwananzila ametoa siku saba kwa wazazi na walezi wote kuwapeleka  shule wanafunzi waliochaguliwa na kutakiwa kuanza masomo ya kidato cha kwanza mwaka huu 2014.
Agizo hilo amelitoa kwa nyakati tofauti wakati anazungumza na wananchi wa kata ya Kikulyungu, Barikiwa, na Mpigamiti alipokuwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo wilaya himo. 
Mhe. Mwanazila alisema elimu ni suala muhimu kwa mtoto ambalo halitakiwi kufanyiwa mchezo hivyo basi mzazi,mlezi atayekaidi agizo hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwa pamoja na kufikishwa mahakamani.
Alisema maendeleo hayawezi kupatikana kila ya elimu hivyo basi elimu ndiyo msingi wa kila jambo kwa kulitambuan hilo ndiyo maana serikali sikivu imeanzisha mpango wa shule za sekondari za kata nchini. 
 Awali mkuu wa wilaya Liwale Mhe. Ephraim Mmbaga alisema katika wilaya yake wanafunzi 1154 wamechaguliwa kujiunga na shule za sekondari mwaka huu lakini hadi sasa wanafunzi 482 tu waliofika katika shule walizopangiwa
Mhe Mmbaga alisema wanafunzi 672 hawajafika shuleni kwa sababu ambazo sio za msingi hali ambayo inatishia na kukatisha tamaa katika ustawi wa maendeleo ya elimu wilaya humo,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...