Kampuni ya bia ya Tanzania (TBL) kwa ushirikiano na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) leo tumezindua rasmi msimu mwingine wa Tuzo za Muziki Tanzania zinazojulikana kama KTMA.

Mkutano na wana habari za michezo na burudani kutoka vyombo mbali mbali ndio umezindua msimu huu katika hoteli ya Kebby’s ilioko maeneo ya Mwenge jijini Dar es Salaam. Viongozi wa BASATA pamoja na wa bia ya Kilimanjaro walizungumzia mabadiliko chanya katika mchakato wa mwaka huu ikiwa ni juhudi na hatua za kuendelea kuboresha mfumo wa upatikanaji wa wateule wa vipengele mbali mbali vya tuzo hizi.

Mabadiliko:
Mwaka huu watanzania wamepewa fursa ya kupendekeza wasanii, nyimbo, vikundi, watayarishaji, video n.k wanazodhani zinastahili kuwepo kwenye mchakato wa kuwapata wateule wa tuzo za muziki Tanzania. Kwakutumia mfumo wa SMS na mtandao wapenzi wa muziki wataweza kutoa mapendekezo yao kupitia;

a. Namba ya simu 15440.
b. Mtandao – Website/tovuti na barua pepe/email.

Semina fupi ilioendeshwa katika hoteli ya Kebbys ilitoa ufafanuzi wa jinsi ya kutoa mapendekezo na wapi mpenzi wa muziki anaweza kwenda kupata maelezo ya ziada yanayohusiana na njia za kutumia kupendekeza kazi na wasanii wanaowataka.

“Baada ya tathmini ya mwaka jana, tumeonelea wakati wa kuwahusisha wapenzi wa muziki umewadia. Tuzo za muziki ni mchakato endelevu unaoendelea kubadilika kila mwaka ikiwa ni jitihada za kuboresha na kuhakikisha mfumo unakua imara, kuhakikisha tunapata wateule na washindi wanaostahili’. Alisema George Kavishe meneja wa bia ya Kilimanjaro.

‘Kama una amini msanii unaempenda ama kikundi ama wimbo n.k inastahili kuingizwa kwenye mchakato, basi pendekeza.’ Alisema George.

BASATA waliwapongeza TBL kwa kuendelea kuwa wabunifu na kuwa makini na tathmini pamoja na taarifa mrejesho (feedback) za wapenzi wa muziki na kuendelea kuzifanyia kazi alimradi kuboresha mfumo mzima wa tuzo hizi za kitaifa.

“BASATA ilipewa nafasi ya kutathmini mchakato huu mpya na tumeuridhia na kuonelea ni mfumo mzuri wenye tija na utakaoleta matoke mazuri zaidi kwa mchakato wa tuzo hizi.” Alisema mwakilishi wa BASATA.

Taarifa kamili za njia ya kupendekeza zipo kwenye mtandao wa Kili http://www.kilitime.co.tz/ktma pamoja na page ya facebook ya Kilimanjaro na kwa taarifa unaweza kuifata handle ya kili @kilimanjarolarger kwenye twitter.

Usiku wa tuzo unatazamiwa kuwa ni tarehe 3-Mei-2014 katika ukumbi wa Mlimani City.

Kwa taarifa zaidi wasiliana na wasimamizi wa taarifa na mchakato wa KTMA, 1Plus kupitia anuani ilioainishwa hapo chini au na George Kavishe, meneja wa Kilimanjaro. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...