Moja ya picha mbalimbli za Tembo zilipamba ukumbi yalipofanyika majadiliano kuhusu tembo, picha hizo na ambazo zilikuwa kivutio kwa washiriki wa majadiliano hayo ziliandaliwa na National Geograpy.
Mkurugenzi Mtendaji wa ABC HOME Paulette Cole akiwakaribisha wanajopo na wageni waalikwa katika majadiliano kuhusu tembo, majadiliano hayo yalifanyika siku ya jumanne usiku Jijini New York.
Chelsea Clinton, Makamu Mwenyekiti wa Clinton Foundation, na ambaye aliongoza majadiliano hayo akiwatambulisha wanajopo, kutoka kushoto ni Bw. John Heminway, Balozi Tuvako Manongi, kati kati ni Chelsea Bint wa Rais Bill na Hilary Clinton, kulia kwa Chelsea ni Bw. Bryan Christy na anayefuatia ni Bw. Josh Ginsberg kutoka Wildlife Conservation Society. Heminway na Christy ni waandishi na watunga filamu na kwa pamoja wametengeneza filamu ijulikanayo kama "The Battle for Elephants". Filamu hiyo itaonyeshwa February 27 kupitia Channel ya National Geograpy.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...