Polisi  wamemakamata  mwenyekiti wa chama cha  waandishi wa habari  mkoa  wa Iringa (IPC) Frank Leonard (wa nne kushoto)  wakimtuhumu kupiga  picha mahakamani. Hadi  sasa amewekwa  chini ya ulinzi wa polisi huku kesi ya mtuhumiwa wa mauwaji ya Mwangosi ikiendelea kusomwa.  
Habari mpya zinasema  askari  wa  jeshi la polisi mkoa  wa  Iringa  wamemwachia huru  Frank Leonard  aliyekamatwa ndani ya  chumba  cha mahakama  wakati akifuatilia mwenendo wa  kesi ya mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwenyekiti wa IPC Marehemu  Daudi Mwangosi.
Polisi hao  wamemwachia  huru  Leonard  baada kwa kile kinachosadikiwa kutokuwa na   ushahidi  kuwa  amepiga picha mahakamani wakati mtuhumiwa  wa mauwaji hayo ambae ni askari polisi akisomewa mashtaka yake.
Mwanahabari huyo amesema yeye hakuwa amewasha kamera yake mahakamani hapo  bali alikuwa ameshika simu yake kabla ya askari mmoja  kusimama na kumkamata ndani ya mahakama  wakati  kesi hiyo ikiendelea. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. SHERIA IPI INAZUIA KUPIGA PICHA MAHAKAMANI? AU KUNA ZUIO LOLOTE LA KISHERIA LIWEKWA? MANAKE DEMOKRASIA NI PAMOJA NA UHURU WA WATU KUJUA KINACHOENDELEA, YANI UWAZI

    ReplyDelete
  2. wewe wa kwanza sema unachotaka kusema usibwabwaje tu. unadhani kila kitu sheria? Taratibu pia hufunga(bind) mtu. Upinzani kila kitu. Unaboa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...