AFISA MSAMBAZAJI WA TANROAD AFARIKI 
DUNIA KATIKA AJALI YA BARABARANI MKOANI MBEYA.

GARI LISILOFAHAMIKA NAMBA ZAKE ZA USAJILI WALA DEREVA WAKE LILIMGONGA MPANDA PIKIPIKI AITWAYE ANDREW CHIWINGA (50) AFISA MSAMBAZAJI WA TANROAD NA MKAZI WA IWAMBI MBEYA ALIYEKUWA ANAENDESHA PIKIPIKI YENYE NAMBA ZA USAJILI STK 8793 AINA YA TVS STAR NA KUSABABISHA KIFO CHAKE PAPO HAPO. 
AJALI HIYO ILITOKEA MNAMO TAREHE 08.02.2014 MAJIRA YA SAA 20:45HRS USIKU ENEO LA IYUNGA WILAYA YA MBEYA VIJIJINI. CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA, MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. 
DEREVA ALIKIMBIA PAMOJA NA GARI MARA BAADA YA TUKIO HILO. JUHUDI ZA KUMTAFUTA ZINAENDELEA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI ALIPO MTUHUMIWA WA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI AKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE, VINGINEVYO AJISALIMISHE MWENYEWE. 
                                                      Signed by:
 [AHMED Z. MSANGI – SACP]

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...