DSCF2810Kulia ni mgeni rasmi Adam Shayo,ambaye ni mkurugenzi wa Taasisi ya elimu ya Sila(SILA VOCATION TRUST ARUSHA) katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu katika  mahafali ya kwanza  chuo cha Biashara na Teknohama Arusha. kushoto ni mkurugenzi wa chuo hicho Valentune Ndanu

Na Pamela Mollel,Arusha.

Wahitimu katika chuo cha Biashara na Teknohama Arusha (IBICTA) wametakiwa kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa kutafuta masoko nje ya nchi kwaajili ya kutangaza  bidhaa za Tanzania hali itakayo saidia  uchumi wa Taifa kuwa juu

Wito huo ulitolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Sila( SILA VOCATION TRUST ARUSHA) Bw. Adam Shayo juzi wakati alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya kwanza chuo cha Biashara na Teknohama Arusha

Alisema kuwa changamoto kubwa iliyopo ni pamoja na bidhaa za Tanzania kutotambulika katika soko la kimataifa huku akidai kuwa asilimia kubwa ya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini zinaubora ukilinganisha na nchi zingine

Aidha aliwata wahitimu kutumia  stashahada zao katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kutafuta masoko nje ya nchi kwaajili ya bidhaa zinazozalishwa hapa Nchini

Kwa upande wake Mkurugenzi wa chuo hicho Bw.Valentune Ndanu alisema kuwa waliohitimu  katika chuo hicho ni wanafunzi 10 huku akidai kuwa elimu waliyoipata  wahitimu hao itawawezesha kufanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu 

Pia alitaja faida nyingine  watakayofaidika nayo ni pamoja na kutambua fursa  zilizopo sanjari na kujiingiza katika ujasiriamali hali itakayowasaidia kuwa na ajira ya kudumu

Malengo ya chuo hicho ni kutoa digrii ya biashara na teknohama hali itakayosaidia vijana kujiingiza katika ujasiriamali,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...