Na Abdulaziz Video,Mnazi Mmoja ,Lindi.

Sekta ya Habari Imetakiwa kutoa elimu zaidi ya ukatili wa Kijinsia ili kujenga Taifa lenye amani kwa wananchi Bila kujali Jinsia ,Dini na kabila.

Wito huo umetolewa na Dr Monica Mhoja , Naibu Mkurugenzi wa mradi wa Champion unaofadhiliwa na Usaid alipokuwa akitoa mada katika warsha ya wanahabari wa Mkoa wa Lindi inayoendelea katika Ukumbi wa Sakina Mnazi mmoja Manispaa ya Lindi.

Dr Mhoja amebainisha kuwa sekta ya habari ina wajinu mkubwa kwa kushirikiana na serikali na mashirika yanayotoa elimu juu ya Unyanyasaji kijinsiaNchini ili kuwapa mwanga jamii kuweza kuchukia vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na haki za Binadamu.

Wanahabari ni jukumu lenu kutoa hii kwa kuwa mnayo nafasi na fursa kubwa ya kuelimisha kwa kuwa vitendo hivyo vinaongezeka kila siku ikiwemo kupigwa,Ukeketaji na ndoa za utotoni ili kuondoa ubaguzi na ukatili huo na hivyo kupitia warsha hii matarajio ya Shirika la Champion ni kuondoa hali hizo kwa kupitia vyombo vya Habari ndio maana tumewakusanya kuwapa elimu,Alimalizia Dr Mhoja.

Lengo la warsha hiyo ni kuwajengea Uwezo na Uelewa wa sheria na sera za Nchi zinazohusisha masuala ya ukatili wa kijinsia.

Warsha hiyo pia Inaendeshwa na Ofisa mradi mwandamizi wa kutoka kitengo cha mawasiliano mradi wa Champion,Bw Muganizi Mutta na tayari mafunzo hayo yametolewa kwa Wanahabari wa mkoa wa Mtwara.
Naibu Mkurugenzi wa mradi wa champion akitoa mada kwa wanahabari wa mkoa wa Lindi katika warsha inayoendelea.
Baadhi ya wanahabari wa Lindi wakiwa katika warsha ya ukatili wa kijinsia inayotolewa na mradi wa Champion
Picha ya pamoja kati ya Naibu Mkurugenzi wa Mradi wa Champion na wana habari wa mkoa wa Lindi waliohudhuria warsha kuhusiana na sheria na Sera za ukatili wa kijinsia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...