1. Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kushoto) akihojiwa na Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha CCTV Zhang He jijini London ambapo alipata nafasi ya kuzungumzia juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika Vita Dhidi ya Ujangili nchini na Changamoto zinazohitaji kuungwa mkono na Jumuiya ya Kimataifa.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akipongezwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Wanyamapori Paul Sarakikya mara baada ya kumaliza mahojiano katika kituo cha BBC jijini London alipokuwa akihudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Biashara Haramu ya Wanyamapori. Kulia ni Katibu wa Waziri Imani Nkuwi.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kati) alipata fursa ya kukutana na Mwandishi wa Gazeti la Daily Mail la Nchini Uingereza Martin Fletcher (kulia) na kumfafanulia juu ya juhudi za serikali katika kupambana na ujangili nchini. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Wanyamapori Paul Sarakikya.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akihojiwa na Mtangazaji Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) Zawadi Machibya ambapo alipata nafasi ya kuzungumzia juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika Vita Dhidi ya Ujangili nchini na Changamoto zinazohitaji kuungwa mkono na Jumuiya ya Kimataifa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe. James Lembeli (kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi wa Wanyamapori Paul Sarakikya (kulia) jijini London walipohudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Biashara Haramu ya Wanyamapori. Kati ni Katibu wa Waziri Imani Nkuwi. 
Picha na Pascal Shelutete, TANAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...