Wachezaji 31 wameteuliwa kujiunga na timu ya Taifa
ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) kwa ajili ya michuano
ya Afrika ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Senegal.
Ngorongoro Heroes itakayokuwa chini ya Kaimu Kocha
John Simkoko akisaidiwa na Mohamed Ayoub inaingia kambini kesho (Machi 19 mwaka
huu) jijini Dar es Salaam kujiandaa kwa mechi ya kwanza dhidi ya Kenya
itakayochezwa kati ya Aprili 4-6 jijini Nairobi.
Kikosi kinachounda timu hiyo ambayo itarudiana na
Kenya kati ya Aprili 25-27 mwaka huu jijini Dar es Salaam kinajumuisha pia
baadhi ya wachezaji walioonekana katika mpango wa ung’amuzi wa vipaji kwa ajili
ya maboresho ya Taifa Stars.
Wachezaji walioitwa ni makipa Aishi Manula (Azam),
Hamad Juma Hamad (Scouting- Temeke), Manyika Peter Manyika (Scouting- Ilala) na
Mwinyi Hassan Hamisi (Mtende, Zanzibar).
Mabeki wa pembeni ni Ayoub Semtawa (Coastal Union),
Edward Charles (JKT Ruvu), Frank Linus Makungu (Scouting- Rukwa), Gabriel
Gadiel Michael (Azam), Hussein Mkongo (Ashanti United) na Ibrahim Said Mohamed
(Chuoni, Zanzibar). Mabeki wa kati ni Bashiru Ismail (Tanzania Prisons), Faki
Rashid Hakika (Ashanti United) na Pato Ngonyani (Majimaji).
Viungo ni Ally Nassoro (Coastal Union), Bryson
Raphael (Azam), Farid Musa (Azam), Hamid Mohamed (Mbeya City), Hassan Mbande
(Mtibwa Sugar), Ibrahim Mohamed Ibrahim (Scouting- Ilala), Idd Seleman (Ashanti
United), Mohamed Issa Juma (Acudu, Afrika Kusini), Muhsin Ally Muhsin
(Scouting- Kinondoni), Seleman Magoma (Scouting- Ruvuma) na Tumaini John
(Scouting- Mwanza).
Washambuliaji ni Ally Salum Kabunda (Ashanti
United), Ibrahim Hamad Hilika (Zimamoto, Zanzibar), Jafari Mwambusi (Mbeya
City), Kelvin Friday (Azam), Ramadhan Bilal (Mlale JKT), Salum Abdilah Mineli
(Ndanda) na Sibiank Lambard (Tanzania Prisons).
YANGA, AZAM KUUMANA VPL TAIFA
Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea
kesho (Machi 19 mwaka huu) kwa mechi kati ya Yanga na Azam itakayochezwa Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni.
Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo zitaanza kuuzwa saa
2 asubuhi katika magari maalumu kwenye vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin
Mkapa, Ubungo Terminal, mgahawa wa Steers uliopo Mtaa wa Samora/Ohio, OilCom
Ubungo, Buguruni Shell, Dar Live- Mbagala, kituo cha daladala Mwenge na Uwanja
wa Taifa.
Baada ya saa 6 mchana mauzo yote yatahamia Uwanja
wa Taifa ambapo milango kwa ajili ya mechi itakuwa wazi kuanzia saa 7.30
mchana.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 30,000 kwa
VIP A, sh. 20,000 kwa VIP B na C wakati viti vya rangi ya chungwa, bluu na
kijani kiingilio ni sh. 7,000.
Mechi hiyo itachezeshwa na mwamuzi Hashim Abdallah
wa Dar es Salaam ambapo atasaidiwa na Anold Bugado (Singida), Florentina Zablon
(Dodoma) na Lulu Mushi (Dar es Salaam). Kamishna wa mechi hiyo Emmanuel Kavenga
kutoka Mbeya wakati mtathimini wa waamuzi ni Alfred Rwiza wa Mwanza.
Boniface Wambura Mgoyo
Media and Communications Officer
Tanzania Football Federation (TFF)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...