Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akibadilishana Mkataba wa Uwekezaji katika shughuli za Kilimo na Ufugaji na Mwekezaji toka Nchini Uturuki ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya TARBIM LTD. Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Magereza limetiliana saini Mkataba huo ambao utatekelezwa katika Shamba la Magereza lililopo Bagamoyo, Mkoani Pwani.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja( meza kuu mbele) akisaini Mkataba  wa Uwekezaji katika shughuli za Kilimo na Ufugaji na Mwekezaji toka nchini Uturuki, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya TARBIM LTD, Bw. Baddal Calikusu(wa kwanza toka kulia). Hafla fupi ya  utilianaji saini Mkataba huo umefanyika Machi 17, 2014 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Kampuni ya TARBIM LTD(kulia mbele meza kuu) akiagana rasmi na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kushoto mbele meza kuu) mara baada ya hafla fupi ya utilianaji saini wa Mkataba wa Uwekezaji katika shughuli za Kilimo na Mifugo ambapo Jeshi la Magereza kupitia Shirika lake la Magereza litatekeleza miradi ya Uzalishaji ya Kilimo na Ufugaji katika Shamba la Magereza lililopo Bagamoyo, Mkoani Pwani kwa kushirikiana na Kampuni ya Mwekezaji ya TARBIM LTD(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza)
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja(mbele meza kuu) akitoa utambulisho wa Makamishna wa Jeshi la Magereza(waliopo kushoto)kwa Mwekezaji wa shughuli za Kilimo na Ufugaji kabla ya kutiliana saini Mkataba wa Uwekezaji wa masuala ya Kilimo na Ufugaji katika Shamba la Magereza lililopo Bagamoyo, Mkoani Pwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...