Ankal naomba nipe nafasi nitangaze nia
yangu ya kuanzisha kampeni ya kupambana na UKUDA hapa Tanzania. Ruksa
kunisahihisha bila kuchafua hali ya hewa; ila nielewavyo mimi UKUDA ni hali ya
kuwa na roho mbaya, roho ya kwa nini, kukatishana tamaa, na pia kutopenda
maendeleo ya wengine - wakati MKUDA mwenyewe akibakia kama alivyo.
Kwa mtazamo huo huo, MKUDA ni mfuasi wa
hayo mambo niliyotaja hapo juu. Na ndio kampeni hii itakapoelekezwa, na
nitahitaji sana msaada wa mawazo ya wadau wa namna ya kuendesha kampeni hiyo
kwa faida ya nchi yetu inayoelekea kupata katiba mpya ambayo naomba UKUDA
usipewe nafasi kabisa kabisa!
Ingawa ni kweli sio wote, lakini si uwongo
kwamba Watanzania wengi ni WAKUDA. Mifano ni mingi sana kiasi naweza kujaza
blog nzima na nisiwe nimetaja japo robo yake tu. Lakini kwa faida yenu naomba
nitoe mifano michache.
UKUDA NA WAKUDA KAZINI
Huko kazini utakuta mtu anaandamwa na
wakuda kwa sababu anapenda kazi yake, anawahi kazini kila siku, anapiga mzigo
kama kwamba ndio siku yake ya kwanza kazini na mabosi wote wanampenda. Hapo
utakuta wafuasi wa UKUDA wanamwandama as
if kaua mtu. Wanamwita mtaka sifa,
anajipendekeza, hana lolote na kadhalika. Mradi inakuwa taabu kuwa mchapa kazi
hodari kwa kuwa WAKUDA hawataki uwe hivyo.
Mbaya zaidi hao WAKUDA wao ni wategaji
wakubwa kazini, wachelewaji na fitina haziwaishi kuwachongea wenzao ambao
hawana tabia kama zao. Pia WAKUDA ni wajuaji wa kila kitu, wabishi wa kila
jambo na daima utawakuta wanapanga njama za kukatisha tamaa asiye kama wao.
UKUDA NA WAKUDA MICHEZONI
Hapa napo hakuna tofauti na kazini.
Mchezaji wa timu Fulani anajituma kwa kuwahi mazoezini, kufanya mazoezi ya
ziada (baada ama kabla ya mazoezi rasmi na wengine), ana nidhamu kwa viongozi,
wachezaji wenzie na hata mashabiki. Huyu naye haachwi na WAKUDA.
Watampachika majina kibao ikiwa ni pamoja
na mtaka sifa, anajipendekeza apangwe kila siku. WAKUDA hao wanataka awe kama
wao ili timu ikishindwa iwe lawama kwa wote.
UKUDA NA WAKUDA MITAANI
Huko nako ndio usisema. Mtu anaamua kuwa
msafi, anafagia kila sehemu ya nyumba yake. Na kama ni nyumba ya kupanga
anahakikisha usafi na unadhifu ni vya lazima kwake. Anaheshimu kila mtu mtaani
na wala hajiingizi kwenye migogoro ya ‘Kiswahili’ , na pia kwenye kila shughuli
iwe ya msiba ama harusi hakosekani. Kama hawezi kuhudhuria anatoa udhuru na
mapema na atahakikisha anawakilishwa na mtu wa familia yake.
Huyu mtu naye unaweza ukamuonea huruma hapo
mtaani ama katika nyumba anayoishi, kwa sababu zile zile za KIKUDA.
HITIMISHO
Kama niliyodokeza, mifano ni mingi mno. Ila
kwa hiyo mitatu nahisi mada yangu hii inaeleweka sasa. Kifuatacho ni kuomba
mawazo ya nini kifanyike ili kampeni ianze. Nimejiandaa kuifanya kampeni hii
kupitia vyombo vya habar vyote, mikutano ya hadhara na makongamano. Wafadhili
kadhaa nilioongea nao wameonesha nia kubwa ya kusaidia kampeni hii ifanikiwe kwa faida ya wote.
Naomba kuwakilisha
MPINGA UKUDA NA WAKUDA
Haaa haaa.Nchi haiendelei kwa mtu anayejituma sana kazini na kila idara kwa Tanzania huwa hapendwi.Atapewa majina ya kila aina kama uluvyosema hapo juu...Uvivu unasumbua watu
ReplyDeleteUvivu ndiyo chimbuko lake.
ReplyDeleteSio uvivu ni tabia iliyojitokeza katika kipindi cha ujamaa na kujitegemea. Kila mtu alishindwa kuchukua jukumu la kuendeleza nchi tukisubiri kufanyiwa ama na serikali ambayo alikuwa ni baba wa taifa tu. Kila mtu aliona si kazi yake kufanya jambo la maendeleo.
ReplyDeleteKwa upande wangu wakuda waliwahi kunifanya nipoteze kazi yangu kwa jambo ambalo sijafanya kabisa na kunichongea kwa boss ambae nae aliyachukua maneno kama yalivyo bila ya uchunguzi si unajua tena kazi za muhindi!
ReplyDeleteMleta mada nikupo hongera na pole kwa wakati mmoja. Hongera kwa kugonga ikulu, maana watanzania, kama ulivyosema, wengi ni wakuda. tembelea katika hoteli ama duka lolote uone wafanyakazi walivyonuna na kufanya kazi kama hawataki vile ama kama wamelazimishwa. si nia yao kuwa hivyo. Ni wakuda waliowazunguka. wakifanya kazi kwa tabasamu na kujituma watapambana na waumimini wa ukuda. Hahaaaaaaa hii mada tamu kweli na inawafaa sana watanzania. Ona wenzetu wakenya. wao ni kazi tu hakuna ukuda. ndio maana wakiwa mabosi hapa bongo wanachukiwa (na wakuda) kwa kuchapa kazi bila noma.
ReplyDeleteNakupa pole kwa kuwa hata sijui utafanikisha vipi kampeni yako maana ukuda upo kila mahali. Ila usikate tamaa. mradi umeanza kwa hatua hii, zingine zitafuatia. Ushauri wangu ni kwamba endeleza hii kasi ya kuupigia kelele ukuda na wala usichoke.
Wakati mwingine siy ukuda ni kuelezwa ukweli unadhania unaonewa wivu, kuna kitu kinaitwa constructive criticism au feedback ambayo unapaswa uipokee kwa kufaraha na kujirekebisha badala ya kuitumia fursa hiyo vizuri unakataa ushauri.
ReplyDeleteWewe anony wa hapo juu unayesema kuelezwa ukweli una harufu ya uumini wa ukuda. constructive criticism inakuaje valid unapomsimanga mwenzio anayejituma na kumwita mtaka sifa? Unajua maana ya maneno hayo kweli ama umeielewa mada? Rudia kuisoma mada yote kisha angalia katikati ya mistari, if u know what i mean. Kinachoongelewa hapa ni nyie wakuda mnaomuona mchakarikaji kuwa ni mtaka sifa, anajipendekeza etc. na si vinginevyo
ReplyDelete