Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akiwa amemuinua mkono Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete ikiwa ni ishara ya kumnadi kwa wananchi wa Kata ya Ubena Zomozi huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha,wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM zinazoendelea katika Kata mbali mbali ndani ya jimbo la Chalinze.

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi na wanaCCM wa Kata ya Ubena Zomozi huku akishangilia kwa shangwe,leo Machi 24,2014.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete akimwaga sera zake kwa Wananchi wa Kata ya Ubena Zomozi wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM zinazoendelea katika Kata mbali mbali ndani ya jimbo la Chalinze.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana (katikati) akiwa amesimama kusikiliza kwa makini sera za  Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete (hayupo pichani) alizokuwa akitoa kwa Wananchi wa Kata ya Ubena Zomozi huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha,wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM zinazoendelea katika Kata mbali mbali ndani ya jimbo la Chalinze.
Wananchi wa Kata ya Ubena Zomozi wakifatilia kwa makini sera za Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete huku wakiwa wamejikinga kwa mvua kwa kutumia viti,wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM zinazoendelea katika Kata mbali mbali ndani ya jimbo la Chalinze.
Wananchi wa Kata ya Ubena Zomozi wakiwa wamejikinga kwa mvua chini ya paa la moja ya Nyumba zilizopo kwenye Kata hiyo wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM zinazoendelea katika Kata mbali mbali ndani ya jimbo la Chalinze.Picha zote na Othman Michuzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Huu ni ubunifu wa haina yake. Viti vinageuzwa chini juu visiloane na wakati huo huo vinatumika kama miamvuli.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...