Mkurugenzi wa Mradi ya Usalama Barabarani wa Shirika
la Transaid la Nchini Uingereza, Mr. Neil Rettie (mwenye tai ya blue)
akimkabidhi funguo za gari aina ya Iveco kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi,
Dkt Shaaban Mwinjaka kwa ajili ya mafunzo ya Udereva yanayotolewa na Chuo Cha
Taifa Cha Usafirhsaji (NIT), Hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya chuo
hicho leo Asubuhi.
Taswira ya tanker
trailer la futi 40 na Folk Lift
ambayo yamekabidhiwa kwa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) na Kampuni ya
Transaid leo asubuhi katika viwanja vya chuo hicho. Magari hayo yatasaidia
wanafunzi wanaosoma kozi za udereva chuoni hapo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya
Uchukuzi, Dkt Shaaban Mwinjaka, akiwasha gari aina ya Folk Lift lililokabidhiwa kwa Chuo Cha Taifa Cha Usarifshaji (NIT),
kwa ajili ya wanafunzi wataochukua mafunzo ya udereva chuoni hapo. Magari hayo
yamekabidhiwa leo asubuhi katika viwanja vya Chuo hicho.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka akijaribu gari hilo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban
Mwinjaka (kushoto), akimsikiliza Mkuu wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT),
Dkt. Zakaria Mganilwa ofisini kwake kabla ya kupokea magari mawili ambayo yamekabidhiwa
kwa chuo hicho na Shirika la Transaid la nchini Uingereza, hafla ya kukabidhi
magari hayo imefanyika leo asubuhi katika viwanja vya NIT.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...