Na  Francis Godwin Blog 
WANANCHI  wa Ludewa  mkoani  Njombe  wamempongeza  Rais Dr Jakaya Kikwete kwa  hatua  yake ya  kuwashirikisha  wananchi wa maeneo husika katika suala la utatuzi wa mgogoro wa mpaka  kati ya Tanzania na Malawi

Hatua  ya  wananchi  hao  kumpongeza  Rais  Dr Kikwete  imekuja  huku  ikiwa ni  siku  tatu zimepita  toka  mbunge wao  wa jimbo  la Ludewa Deo Filikunjombe ,mbunge wa jimbo la Kyela Dk. Harrison Mwakyembe na mbunge wa   jimbo la Mbinga  Magharibi John Komba  kurejea nchini  kutoka Malawi  katika  kikao  cha usuluhishi  wa mgogoro  wa mpaka kati ya Malawi na Tanzania

Wakizungumza na  mwandishi  wa habari hizi wananchi hao  akiwemo Yohana  Haule  walisema  kuwa  hatua  ya  Rais Kikwete  kutumia  wananchi  wenye  kushughulikia  suala  hilo  ni hatua ya  kupongezwa  kwani wabunge hao  ni wawakilishi wa  wananchi hivyo kila kinachoendelea kitawafikia mapema  wananchi  wa maeneo ya mpakani Malawi na Tanzania.

Haule  alisema  kuwa  imani na matumani  ya  wana Ludewa ni kuona mbunge  wao amewawakilisha  katika  suala hilo na  kuwa  hawana  shaka na uwakilishi  wake na wanaamini  watapewa mrejesho  wa  kila kinachoendelea  katika  suala  hilo.

Hivyo  alisema  kwa  sasa hofu  ambayo awali  wananchi wa kando ya  ziwa Nyasa  walikuwa nayo  juu ya mgogoro  huo wa mpaka kati ya  Tanzania na Malawi  imeanza  kutoweka  kutokana na mbunge  wao Filikunjombe kuzunguka maeneo  yote ya Mwambao na  kufanya  mikutano na  kuwaondoa hofu  juu ya  hilo.

Huku Sarah Haule  mbali  ya  kumpongeza  Rais  Kikwete kwa  hatua  hiyo  pia  alimpongeza mbunge  Filikunjombe kwa jitihada mbali mbali  za  kuwaletea  maendeleo  wananchi  wa Ludewa  huku  akimtaka  mbunge   huyo kuendelea  na msimamo  wake  katika kuwawakilishi  wana  Ludewa bungeni .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...