Rais wa Tanzania Red Cross, Dr. George Nangale,  akifurahia jambo wakati akipokea mfano wa hundi ya Shilingi Milioni kumi kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha kusaidia jamii" Vodacom Foundation" Yessaya Mwakifulefule. Fedha hizo zimetolewa kwa chama hicho kwa ajili ya kuimarisha huduma na kusaidia waliokumbwa na maafa ya mafuriko yaliyotokea Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro na kuacha mamia ya kaya bila makazi. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Maendeleo wa Chama cha Msalaba Mwekundu, Julius Kejo na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania,Salum Mwalimu.
 Rais wa Tanzania Red Cross, Dr. George Nangale,  akisisitiza jambo kwa waandishi wa Habari (Hawapo pichani) punde baada ya kupokea msaada wa fedha, kiasi cha Shilingi milioni kumi kilichotolewa na Vodacom Tanzania kupitia kitengo chake cha kusaidia jamii"Vodacom Foundation" kwa ajili ya kuimalisha huduma na kusaidia waliokumbwa na maafa ya mafuriko yaliyotokea Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro. Pamoja nae katika picha kutoka Kushoto ni Mkuu wa Vodacom Foundation, Yessaya Mwakifulefule na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim.
 Rais wa Tanzania Red Cross, Dr. George Nangale na Mkuu wa kitengo cha kusaidia jamii cha Vodacom Tanzanaia"Vodacom Foundation" Yessaya Mwakifulefule, wakimsikiliza mmoja wa Maafisa wa Tanzania Red Cross punde baada ya kupokea msaada wa fedha kiasi cha Shilingi milioni kumi Kilichotolewa na Vodacom Tanzania kupitia kitengo hicho  kwa ajili ya kuimalisha huduma na kusaidia waliokumbwa na maafa ya mafuriko yaliyotokea Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro
 Mkuu wa Kitengo cha kusaidia jamii cha Vodacom Tanzania" Vodacom Foundation" Yessaya Mwakifulefule akizungumza na  waandishi wa Habari (Hawapo pichani) punde baada ya kutoa msaada wa fedha kiasi cha Shilingi milioni kumi Kilichotolewa na kitengo hicho"Vodacom Foundation"kwa ajili ya kuimalisha huduma na kusaidia waliokumbwa na maafa ya mafuriko yaliyotokea Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro. Pamoja nao katika picha ni Rais wa Tanzania Red Cross, Dr. George Nangale (katikati)Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...