kutoka kushoto Dkt. Grace Mallya kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Bi. Grace Mwangwa Mtaalamu wa masuala ya Jinsia, Wizara ya Fedha na aliyekaa nyuma ni Bi. Constacia Gabusa Kaimu Mkurugenzi -(Jinsia) Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, wakifuatilia hotuba ya Waziri.
Mhe. Sophia Simba ( Mb) Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, akielezea uzoefu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Millenia ( MDGs) ni katika Mkutano wa 58 wa Kamisheni kuhusu Hali ya Wanawake unaoendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Waliokaa pamoja na Mhe. Waziri ni Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi. Bibi. Anna Maembe, Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na Bibi. Asha Ali Abdulla, Katibu Mkuu, Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Ujumbe wa Tanzania unavyoonekana katika ujumla wao, wa kwanza ni Katibu wa Waziri, Bi Teodosia Mbunda akijadiliana jambo na Mhe. Jaji Iman Aboud
Bibi. Mwanaidi Saleh Abdulla, Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bi. Fatma Mbarak Hashim Mtaalam masualaya Jinsia,( Zanzibar), Bw. Seif Shaaban Mwinyi, Kamishna na mratibu wa shughuli za Idadi ya Watu, Tume ya Mipango- (Zanzibar) na aliyekaa nyuma ni Bw. Adam Hans Kadege, Mtakwimu kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Tanzania imewakilishwa vizuri katika mkutano huu kwa kuwa na wajumbe kutoka pande zote za Muungano.
Wajumbe wengine wakifuatilia hotuba ya Mhe. Waziri. Kutoka kushoto, ni Bi. Joyce Mlowe kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi Mhaza Gharibu Juma, Mkurugenzi wa Mipango, Sera na Utafiti, Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto - Zanzibar na Bi. Halima Abdulrahman Omar, Mtaalamu wa Jinsia, Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto- Zanzibar . pamoja na kuhudhuria majadiliano ya mada kuu kuhusu mafanikio na changamoto za utekelezaji wa MGDs, wajumbe wa Tanzania pia wamekuwa wakishiriki kikamilifu katika majadiliano ya mada nyingine nyingi zinazofanyika katika mikutano ya pembezoni ( side-events)
Na Mwandishi Maalum
Wakati Mkutano wa 58 wa Kamisheni kuhusu Hali ya wanawake, ukiwa umeingia wiki yake ya pili, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeeleza kwamba imejitahidi na imefanikiwa kufikia baadhi ya Malengo ya Maendeleo ya Millenia hata kabla ya mwaka 2015.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mhe. Sophia Simba ( Mb) ameyasema hayo siku ya jumatatu wakati Tanzania ilipopata fursa ya kuielezea jumuiya ya kimataifa uzoefu wake katika utekelezaji wa MDGs na changamoto ambazo bado inaendelea kukabilina nazo katika baadhi ya malengo.
Mhe. Sophia Simba, amesema Tanzania imefanya vizuri katika malengo nane kati ya nane ingawa bado inakabiliwa na changamoto katika baadhi ya maeneo ambayo alielezea pia namna serikali inavyojipanga kukabiliana nayo.
Kwa wiki mbili sasa, wawakilishi wa kutoka nchi mbalimbali duniani zinazohudhuria mkutano huu hapa Umoja wa Mataifa, wamekuwa wakipashana habari na wakubadilishana uzoefu kuhusu masuala yahusuyo haki za wanawake, za mtoto wa kike na ustawi wao na maendeleo yao.
Aidha wawakilishi hao wamekuwa pia wakiijadili mada kuu ya mkutano huu ambayo ni mafanikio na changamoto za utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Millennia, ambapo kile nchi imekuwa ikitoka uzoefu wake.
Baadhi ya malengo aliyoeleza kwamba Tanzania imefanya vizuri ni pamoja na lengo namba mbili linalohusu fursa ya elimu ya msingi kwa watoto wote na kwa kuzingatia uwioano wa kijinsia.
Aidha akabainisha pia kwamba Tanzania imefanya vizuri katika lengo la tatu kuhusu fursa sawa za kijinsia na uwezeshwaji wa wanawake ambapo alitolea mfano ongezeko la wanawake katika vyombo vya utoaji maamuzi kama vile Bunge na Baraza la Wawakilishi.
Na katika sekta ya elimu ya sekondari ingawa uwiano huo unapungua kuelekea elimu ya juu
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto akielezea zaidi mafanikio ya utekelezaji wa MDGs, ameeleza pia kwamba kumekuwa na mafanikio ya kuridhisha katika upunguzaji wa vifo vya watoto wachanga chini ya miaka mitano kwa pande zote mbili za Muungano.
Hata hivyo licha ya mafanikio ya kuridhisha katika eneo hilo, Waziri Simba anasema bado watoto wanaendelea kupoteza maisha kwa maradhi yanazulikia kama vile malaria na kuharisha.
Kuhusu lengo namba tano kuhusu upunguzaji wa vifo vya wanawake wajawazito, Waziri anasema, eneo hilo bado linachangamoto nyingi na kwamba kasi yake ni ndogo.
Ametaja baadhi ya changamoto zinazolikabili eneo hili kuwa ni uhaba wa wataalamu, eneo ambalo anasema tayari serikali inalitafutia ufumbuzi, ukosekanaji wa huduma za upasuaji wa dharura eneo ambalo amesema serikali pia inalifanyia kazi kwa kujaribu kuviwezesha vituo vya afya kuwavipatia vifaa na wataalam
Kuhusu lengo la sita linalohusu huduma za afya, Tanzania, kwa mujibu wa Mhe, Waziri, bado inachangamoto nyingi katika kukabiliana na maambukizi ya virusi vinavyosambabisha ugonjwa wa ukimwi, malaria na Kifua kikuu magonjwa ambayo yanagusa sehemu kubwa ya jamii.
Akasema serikali imejitahadi sana katika kuyadhibiti magonjwa haya , kiasi kwamba kumekuwapo na udhibiti wa maambukizo miongoni mwa watu wazima.
Kuhusu lengo namba saba linalohusiana na Mazingigira endelevu, pamoja na huduma za maji safi na salama, Waziri anasema, bado kuna tatizo kubwa la upatikanaji wa maji safi na salama hasa maeneo ya vijijini.
Mhe. Waziri Simba anabainisha kwamba changamoto kubwa kwa Tanzania iko katika utekelezaji wa lengo namba moja, linalohusu utokomezaji wa umaskini uliokidhiri na njaa.
Pamoja na kuelezea mafanikio na changamoto za utekelezaji wa MDGs, Waziri Simba, amesema Tanzania inaunga mkono msimamo wapamoja wa Umoja wa Afrika, unaosisitiza kwamba usawa wa jinsia na uwezeshwaji wa wanawake, uwe lengo linalojitegemea katika Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu baada ya 2015 ( SDGs).
Nafikiri walipeleka wizara yote kwenye huu mkutano. Guys, that is a very very big delegation.
ReplyDelete