Katibu Mkuu wa CCM;Ndugu Kinana na Wananchi wakishiriki ujenzi wa Ghala la kuhifadhi mazao na mashine ya kusaga nafaka katika kijiji cha cha Kidahwe,Kigoma Vijijini.Ghala hilo  linalenga kusaidia katika kuhifadhi mazao ya wakulima na kijiji hicho baada ya kuvuna ili kusubiri soko na bei nzuri ya mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.Usimikaji wa mashine katika ghala hilo utawasaidia  pia wakulima kuchakata mazao yao (hasa mahindi na muhugo) na kuuza unga badala ya mahindi.Gharama za mradi huo ni shiliingi milioni 104,800,000/=.
Katibu wa NEC-CCM wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akishiriki ujenzi wa Ghala la kuhifadhi mazao na mashine ya kusaga nafaka katika kijiji cha cha Kidahwe,Kigoma Vijijini.Ghala hilo  linalenga kusaidia katika kuhifadhi mazao ya wakulima na kijiji hicho baada ya kuvuna ili kusubiri soko na bei nzuri ya mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.Usimikaji wa mashine katika ghala hilo utawasaidia  pia wakulima kuchakata mazao yao (hasa mahindi na muhugo) na kuuza unga badala ya mahindi.Gharama za mradi huo ni shiliingi milioni 104,800,000/=.
Baadhi ya Wazee wa kijiji cha Nkungwe wakifuatilia yaliyokuwa yanazungumwa na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana katika kijiji cha Nkungwe,kuhusiana na tatizo la ufumbuzi wa mradi wa maji.
Mjumbe wa NEC,Balozi Ally Karume akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana mara baada ya kukagua mradi mkubwa wa maji katika kijiji cha Nkungwe,Kigoma vijijini.Mradi huo umeshindwa kukamilika kutokana na ukosefu wa fedha,lakini pia Kinana amewahidi wananchi kulitafutia ufumbuzi wa haraka tatizo hilo na hatimaye mradi huo kukamilika na kuwasaidia wananchi mbalimbali wa maeneo hayo.
Ndugu Kinana akiwasalimia wananchi mbalimbali (hawapo Pichani),wakati alipokuwa akiwasili katika kijiji cha Nkungwe kukagua mradi wa maji ambao umeshindwa kukamilika kutokana na ukosefu wa fedha. Kinana amewaahidi wananachi kulitafutia ufumbuzi suala hilo ili mradi huo ukamilike na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.
Ujenzi wa tanki hilo la maji kama lionekanavyo pichani.
Ndugu Kinana (wa tatu kulia),akishiriki kufukia mabomba ya mradi wa maji katika kijiji cha Nkungwe,Kigoma vijijini.Mradi huo ukikamilika unatarajiwa kusaidia vijiji zaidi ya 30.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisoma orodha ya vijiji vitakavyopatiwa umeme na maji katika wilaya ya Kigoma Vijijini. Kikiwemo Kijiji cha Mahembe ambacho tayari kimepata umeme.
Katibu wa NEC-CCM wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye (katikati) akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Mahembe, Jimbo la Kigoma Kaskazini.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hayo ndio maisha ya watanzania!!!!. Wabunge wa katiba badala ya kuokoa fedha wanataka kuongezewa muda ili waendelee kubishania mambo yasiyokuwa na tija wala msingi. Elekezeni fikra zenu kujenga uchumi wa nchi na si kubishania serikali. Ikiwa na serikali mbili au tatu zitaleta maendeleo? Angalieni uchumi wa nchi acheni mchezo wa vyama na kufikiria madaraka.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...