Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana na baadhi ya viongozi wa chama Wilaya ya Kalambo,wakikatiza kwenye Ofisi ya CHADEMA,ambayo inadaiwa imefungwa yapata miaka mitatu sasa, kwa kushindwa kulipia pango.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akibeba tofali aliyoifyatua,ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa jengo la CCM,wilayani Kalambo.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwahutubia wakazi wa kata ya Kasanga,iliopo ndani ya wilaya mpya ya Kalambo,mkoani Rukwa mapema jana jioni.Kinana bado yupo Mkoani Rukwa na ziara yake ya kuimarisha chama,kukagua miradi mbalimbali,ikiwemo na kusikiliza kero za wananchi. 
Baadhi ya akina mama wakazi wa kata ya Kasanga wilayani kalambo wakishangilia jambo,wakati Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipokuwa akizungumzia mambo mbalimbali ikiwemo utatuzi wa masuala ya  Afya,Elimu,Barabara na maji.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa,Balozi Ally Karume akihutubia mbele ya wananchi wa kijiji cha Kasanga kilichopo kando kando ya Ziwa Tanganyika,Wilayani Kalambo mkoani Rukwa mapema jana,wakati wa mkutano wa hadhara.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizawadiwa zawadi kutoka kwa akina mama wa kata ya Kasanga,iliopo ndani ya wilaya mpya ya Kalambo,mkoani Rukwa.Kijiji cha Kasanga kipo kando kando ya Ziwa Tanganyika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...