Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira masasi-Nachingwea (MANAWASA) inatoa taarifa ya kusikitishwa kwake kutokana na matukio yasiyo ya kiustaharabu yanayoendelea hivi sasa ya wizi wa "MITA ZA MAJI" zilizofungwa na wateja kwenye maeneo wanayoishi ambapo mpaka sasa tayari mita 7 zimeshaibiwa na watu wasiojulikana kwenye mitaa ya MKUTI, JIDA pamoja na REST CAMP.

hivyo Mamlaka ya MANAWASA inawaomba wakazi wote wa mji wa masasi wenye nia njema na huduma hii muhimu kwa wananchi kutoa ushirikiano katika kuwafichua wezi hao na hatimaye wafikishwe mahakamani kwa hatua nyingine za kisheria. 

"EWE MKAZI WA MASASI KUMBUKA KWAMBA HAPO AWALI MASASI HAIKUWA HIVI ILIVYO SASA KWENYE SUALA LA MAJI" Hivyo ni vyema kila mmoja akawa mlinzi wa mwenzake ili kuifanya miundombinu ya MANAWASA iendelee kudumu wakati wote...

pia MANAWASA inatoa wito kwa wale wenye tabia ya kuchimba mchanga karibu na mabomba ya maji kwenye barabara kuu itokayo mtwara kuingia masasi waache mara moja kwani kwa kufanya hivyo husababisha mabomba hayo kupasuka na maji kushindwa kufika Masasi.
Baadhi ya miundombinu ya maji ya Mamlaka (MANAWASA).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...