Na Richard Bagolele,Chato

Mbunge wa jimbo la Chato na waziri wa Ujenzi Mhe. Dk. John Pombe Magufuli leo amekutana na baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato kwenye ukumbi wa Halamshauri na kutoa zaidi ya Shilingi Milioni 80 za mfuko wa Jimbo kwa kila kata kwa style mpya ambapo kila diwani ametaja mahitaji yake na kupewa kiasi hicho kwa ajili ya kukamilisha miradi yenye nguvu za wa wananchi.

Tofauti na miaka mingine ambapo fedha hizo zimekuwa zikitolewa na kamati maalumu ya mfuko wa jimbo ambaye Mhe. Mbunge ni Mwenyekiti wa kamati hiyo.

Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi Mhe. Magufuli amesikiliza hitaji la kila diwani kutoka kwenye kata na kutoa sehemu ya fedha za mfuko wa jimbo ili kusaidia miradi ambayo tayari imeanzishwa kwa nguvu za wananchi.

Madiwani hao walioanza kwa kila mmoja kutaja mahitaji yake hususani miradi ambayo imeanzishwa na wananchi lakini imekwama katika hatua za umaliziaji Mhe. Magufuli alitoa kiasi cha fedha kisichopungua Milioni moja kwa kila mradi ambapo kila diwani alikuwa na miradi zaidi ya mitatu.

“utaratibu huu ni mzuri, nimeamua kukutana na ninyi waheshimiwa madiwani ambao mnatoka kwa wananchi ambako kuna miradi muniambie ili kila diwani anieleze matatizo yake, na nimeona utaratibu huu ni mzuri kwani ningeweza kukaa na wajumbe wangu tukagawa hizi fedha tunavyotaka lakini leo tunagawa bila upendeleo” alisisitiza waziri Magufuli.

Hata hivyo waziri Magufuli amewataka madiwani kwa kushirikiana na watendaji kuhakikisha fedha hizo zilizotolewa na mfuko wa jimbo zinafanya kazi zilizokusudiwa tu na kuwaomba wazisimamie vyema.

Nao madiwani waliopata nafasi ya kuongea wakiwemo wa vyama vya upinzani walimshukuru waziri Magufuli kwa utaratibu huo wa kugawa fedha za mfuko wa jimbo kwa kuwashirikisha madiwani wote tena kwa uwazi mkubwa na wamemwahidi kumpa ushirikiano katika kuleta maendeleo kwa wananchi.

Naye mwenyekiti wa CCM wilaya ya Chato ndugu Ibrahim Bagura amemshukuru Mhe. Magufuli kwa kitendo hicho cha kugawa fedha za mfuko wa jimbo kwa uwazi bila upendeleo wa vyama na kuwaomba madiwani wazisimamie vyema fedha hizo.
Mhe.Dk. Magufuli akisoma taarifa ya fedha ambazo zimewahi kutolewa na mfuko wa jimbo kwa wajumbe wa baraza la madiwani la Halamshauri ya Wilaya ya Chato.
Diwani wa kata ya Muganza Mhe. Michael Maduka akichangia katika kikao hicho.
Wajumbe wa baraza la madiwani wakimskiliza Mbunge wa jimbo la Chato Mhe. Dk. John Magufuli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...