Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dr. Rehema Nchimbi (mwenye kilemba kichwani) akikagua jengo la maktaba mkoa wa Dodoma kujionea mfumo wa vifaa vinavyotumika kutolea elimu na taarifa mbalimbali kwa njia ya video na sauti,  zoezi hili la ukaguzi lilifanyika mapema leo kwenye viwanja vya maktaba ya Dodoma wakati wa maadhimisho  ya miaka 50 ya bodi ya huduma za maktaba
 Watumishi wa maktaba ya mkoa Dodoma wakiwa tayari kupokea wananchi wenye mahitaji mbalimbali ya huduma za maktaba kwa ajili ya kuwapa maelekezo ya namna ya kupata taarifa na huduma nyingine mbalimbali mapema leo wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya bodi ya huduma za maktaba, maadhimisho mkoa Dodoma yalifanyika viwanja vya maktaba ya Dodoma.
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dr Rehema Nchimbi (mwenye kilemba kichwani) akikagua nyaraka na vitabu mbalimbali wakati akitembelea mabanda ya maonesho  ya vitabu wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya bodi ya huduma za maktaba Nchini, maadhimisho mkoa Dodoma yalifanyika viwanja vya maktaba ya mkoa.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dr. Rehema Nchimbi (mwenye kilemba kichwani) akipata ufafanuzi kutoka kwa mtaalamu wa kutafsiri taarifa za vitabu na nyaraka mbalimbali katika lugha za watu wenye mahitaji maalumu/wenye ulemavu wa kuona (nukta nundu) Mwl. Charles Mtimatuku mapema wakati anatembelea mabanda ya maonesho wakati wa hafla ya maadhimisho ya miaka 50 ya bodi ya huduma za maktaba nchini  mkoani Dodoma. Huduma za maktaba nchini zimepiga hatua kiasi cha kuzalisha taarifa na nyaraka mbalimbali kwa watu wenye mahitaji maalumu.NA JOHN BANDA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...