Balozi Ramadhan Mwinyi, Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, akizungumza katika Chemba ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano wa siku moja wa Baraza hilo uliofanyika juzi ( jumatatu) mkutano huo ulihusu mageuzi ya sekta za usalama, ambapo kwa mara ya kwanza Baraza Kuu la Usalama lilipitisha Azimio linalojitegemea kuhusu mageuzi katika sekta za usalama. Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi 42 zilizochangia majadiliano hayo yaliyofunguliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon ambapo hoja iliyozungumzwa na wengi ni umuhimu wa nchi kumiliki mchakato wa mageuzi ya sekta za usalama. Nyuma ya Balozi, ni Lt. Kanali Wilbert Ibuge, Mwambata Jeshi katika Uwakilishi wa Kudumu.
Home
Unlabelled
NCHI ZIMILIKI MAGEUZI YA SEKTA ZA USALAMA - TANZANIA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...