JESHI la Polisi hapa nchini, limeshindwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wa madawa ya kulevya katika mkoa wa Manyara, ambapo kwa sasa Polisi wamekamata misokoto ya bangi 2,676 na mirungi bunda 70 katika mkoa huo, huku likishindwa kakabiliana na hali hiyo kutokana na Askari wake kushiriki vitendo hivyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Bangi1
Aidha kumbukumbu zinaonyesha kuwa katika kipindi cha Machi, mwaka 2012, Jeshi hilo mkoani Kilimanjaro lilimshikilia Askari wake (G 842, Konstebo Deogratius), ambaye alikamatwa na misokoto mine ya bangi akiwa katika ukumbi wa disko wa Albeto uliopo mjijni Moshi, huku akifanya vurugu katika ukumbi huo ambapo pamoja na Jeshi la Polisi mkoani humo kuthibitisha tukio hilo, mtuhumiwa huyo akisukwa rumande pamoja na Askari mwingine ambaye aliingia katika ukumbi huo akiwa na bunduki aina ya SMG na kufanyia watu fujo.
Mbali na matukio hayo Jeshi hilo, lilitoa taarifa ya kukamata kwa watuhumiwa 45 wakihusishwa na matukio ya utumiaji wa bangi, mirungi na gongo katika msako wa kuimarisha doria katika maeneo mbalimbali mkoani humo, msako ambao hadi leo Polisi mkoani humo wameshindwa kuwafikisha makahamani watuhumiwa wakidai bado uchunguzi haujakamilika Globu ya Jamii imebaini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...