Leo Jumatatu, Aprili 7, Redio yako ya Kijamii ya KwanzaJamii imeandika historia kwa kuwa redio ya kwanza hapa nchini kuwaletea wasikilizaji dondoo za habari za magazetini kutokea kwenye soko lenyewe la habari, ni  pale kona ya Uhuru na Msimbazi, Kariakoo.
Ni kipindi cha kila siku kuanzia saa kumi na moja na nusu alfajiri. Mwandishi/ Mtangazaji wa KwanzaJamii atakuwa sokoni hapo na kuungana moja kwa moja na studio za Kwanzajamii radio Iringa.
Sambamba na redio, habari hizo na picha za magazeti yenyewe zitarushwa pia kwenye Mjengwablog.com. Ikumbukwe, Mjengwablog ilikuwa ni blogu ya kwanza hapa nchini kuanza kurusha kwenye blogu dondoo za magazetini.
Usikose kufuatilia na kuzipata habari zikiwa motomoto kutoka Soko la habari Kariakoo...http://www.mjengwablog.com/habari-za-kijamii/item/10489-kutoka-soko-la-habari-kariakoo.html#.U0JH6ldQ7U4

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...