Kamishna wa Huduma za Urekebishaji wa Magereza, Deonice Chamulesile akisoma risala ya ufunguzi katika Kikao cha uwasilishaji wa Stadi juu ya jinsi ya kudhibiti idadi ya Wafungwa Magerezani iliyofanywa na Asasi ya Kiraia ya IRaWS - T. Kikao hicho kimefanyika leo Aprili 30, 2014 katika Ukumbi wa Luther House, Jijini Dar es Salaam(wa kwanza kulia) ni Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Nicas Banzi(wa pili kushoto) ni Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza Onel Malisa(wa kwanza kushoto) ni Katibu Mtendaji wa Asasi ya IRaWS - T, Naibu Kamishna Mstaafu wa Magereza, John Nyoka.
Baadhi ya Watoa Mada mbalimbali wakifuatilia kwa makini uwasilishaji wa Stadi juu ya jinsi ya kudhibiti idadi ya Wafungwa Magerezani(kushoto) ni Afisa Mtafiti Mwandamizi toka Tume ya Kurekebisha Sheria, Prof. Sufian Bukurula.
Mhadhiri toka Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bw. James Jesey(aliyesimama) akiwasilisha rasmi Stadi ya jinsi ya kudhibiti idadi ya Wafungwa Magerezani.
Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wadau mbalimbali waliohudhuria Kikao hicho cha uwasilishaji wa Stadi juu ya jinsi ya kudhibiti idadi ya Wafungwa Magerezani. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Luther House, leo Aprili 30, 2014 Jijini Dar es Salaam(wa kwanza kulia) ni Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya IRaWS - TANZANIA, Kamishna Mkuu Mstaafu Magereza Nicas Banzi(wa pili kushoto) ni Mwenyekiti wa Asasi ya IRaWS - Tanzania, Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza Onel Malisa(wa kwanza kushoto) ni Afisa Mwandamizi Mstaafu wa Magereza, Bi Regina Thomas(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...