Shindano la Mama Shujaa wa Chakula linaloendeshwa na kusimamiwa na Oxfam limefikia tamati ya hatua ya awali ya kutafuta washindi kwa kutangaza wanawake 20 kuingia katika top 20 ya shindano hilo la aina yake.

Wanawake hao wenye wasifu tofauti tofauti sasa wataingia katika kijiji cha maisha plus kwa muda wa wiki tatu ikiwa ni katika hatua ya kutafuta mshindi wa shindano hilo ambalo linalenga kuhamasisha jamii juu ya kilimo, hifadhi ya chakula na namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na njaa. Mbali na wanawake hao 20 pia kuna mshiriki mmoja ambaye yeye amepatikana kwa shindano la mtandaoni.

Hapa nakuletea orodha ya akina mama hao mmoja baada ya mwingine. 
GRACE G.D MAHUMBUKA (46) mkazi wa Karagwe Kagera nambari yake ya ushiriki ni MS 08, ni mkulima wa shamba la ekari 18 na na mfugaji wa ng’ombe, kondoo na mbuzi.


ANADHANI YEYE NI MFANO WA KUIGWA: Kwa sababu anawahamasisha wana kijiji kutumia vyema mvua za kwanza na kupanda miti kwa ajili ya utunzaji wa vyanzo vya maji na kutunza mazingira."Nina shamba lenye ukubwa wa ekari 18. Kwa mwaka ninavuna mazao gunia 35"

BOFYA HAPA KUONA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...