MIMI Hafidh Athumani Kido, nikiwa na akili timamu natangaza kutojihusisha na shughuli zote za Coastal Union, hasa usemaji wa klabu.

Miongoni mwa sababu nyingi zilizonifanya kutangaza uamuzi huo ni sintofahamu iliyozuka ndani ya klabu yetu, kwa taaluma yangu ya uandishi wa habari lazima niwe na msimamo juu ya mambo yanayoendelea kwenye jamii.

Ili niendelee kufanya kazi na klabu hii kwa wakati huu wa misuguano, lazima niwe na upande; kwa maana upande unaounga mkono uongozi ama upande usiokuwa na Imani na uongozi. Lakini mimi nimeamua kutounga mkono upande wowote.

Kwa hivyo basi, ili niwe katika mstari sahihi nimeamua kukaa pembeni nifanye shughuli zangu za uanahabari kwa furaha na amani.

Bado ni mwanachama halali wa Coastal Union Sports Club, namba yangu ya kadi ni 0013. Nitaendelea kutoa ushauri na kuishabikia klabu yangu ambayo nimekuwa nikimuona marehemu baba yangu na kaka zangu wakiishabikia tangu nikiwa mdogo.

Mtashangaa nimetangaza uamuzi huu wa kuachia ngazi bila kusema kuwa nimeandika barua ama la, kifupi sina mkataba wala taarifa yoyote ya kimaandishi juu ya kuajiriwa kwangu na klabu. Hivyo nimeamua kujiuzulu kienyeji kama nilivyoitwa kienyeji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Hongera kaka kwa uamuzi wenye busara

    ReplyDelete
  2. Aisee! MLIKUTANA KIMJINIMJINI NA KUACHANA KIMJINIMJINI!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...