.Kiongozi wa Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  katika Mkutano wa 47 wa  Tume ya Idadi ya Watu na Maendeleo, Bw. Charles Pallangyo, Katibu Mkuu, Wizara ya  Afya na Ustawi wa Jamii,  akizungumza wakati wa  majadiliano ya jumla kuhusu mada kuu ya mkutano huu wa siku  tano kuhusu tathmini ya  utekelezaji wa  Mapango wa Utekelezaji wa Mkutano wa Kimataifa  juu ya Idadi ya Watu na Maendeleo (ICPD) uliofanyika mwaka 1994 huko Cairo, Misri. Wanaooneka nyuma ni   Bw. Noel Kaganda, Afisa wa Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  na Bw.  Stephen  Kiberiti  -Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.Tanzania ni  kati ya nchi 47 zinazounda  Tume  ya Idadi ya Watu na Maendeleo.
 Sehemu ya wajumbe wanaoziwakilisha serikali zao katika mkutano huu. Pamoja na wawakilishi wa serikali,  mkutano huu pia  kutokana na umuhimu wa mada yenyewe   unahudhuriwa na idadi kubwa wajumbe kutoka Asasi zisizo za kiserikali.
 Kutoka na uwingi wa wajumbe na hivyo kuufanya ukumbi  wa mkutano kuwafinyu, wajumbe wengine walilazimika kufuatilia  majadiliano kwa kuangalia kwenye screen katika ukumbi mwingine ( overflow room)  kama wanavyooneka sehemu ya ujumbe wa  Tanzania, kutoka  kulia ni  Bi. Samia A. Diria, Afisa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Ngasuma Kanyeka ( International  Parenthood) Bw. Enock A. Mhehe, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Bi. Vanessa Anyoti ( YWCA)
Wajumbe wengine wa Tanzania kutoka kushoto. Bw.  Edwin M. Minde kutoka Ofisi ya Rais Tume ya Mipango,  Bi. Lulu Ng'wanakilala ( UMATI)   Dkt. Mohameed Dahoma,  Mkurugenzi wa Huduma za Kinga na Elimu ya Afya, Wizara ya Afya -Zanzibar na mjumbe wa mwisho  kutoka United Nations Association. Ujumbe huu wa Tanzania ulikuwa ukishiriki katika majadiliano ya  maandalizi ya Azimio la Mkutano huu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...