Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John P. Magufuli (Mb) akiwakisilisha bajeti ya Wizara ya Ujenzi Bungeni.

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo limepitisha Bajeti ya Wizara ya Ujenzi yenye jumla ya Shilingi 1,219,717,592,000.00 kwa ajili ya matumizi ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2014/15.

Hatua hiyo ya Bunge kupitisha Bajeti hiyo itawezesha Wizara  ya Ujenzi kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuendeleza Sekta ya Ujenzi hapa nchini.

Akiwasilisha hotuba ya bajeti hiyo jana, Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (Mb), alieleza kuwa kati ya fedha hizo Shilingi 557,483,563,000.00 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida ambazo zinajumuisha Shilingi 24,338,319,000.00 za mishahara ya Watumishi (PE), Shilingi 6,944,846,000.00 za matumizi mengineyo (OC) na Shilingi 526,200,400,000.00 kwa ajili ya Mfuko wa Barabara.

Akifafanua kuhusu bajeti ya Maendeleo iliyotengewa Shilingi 662,234,027,000.00, Mhe. Magufuli ameeleza kuwa, kati ya fedha hizo Shilingi 450,000,000,000.00 ni fedha za ndani za miradi ya maendeleo na Shilingi 212,234,027,000.00 ni fedha za nje za miradi ya maendeleo.
   
Wizara ya Ujenzi ina majukumu yafuatayo, Kusimamia Sera za ujenzi na usalama barabarani, Ujenzi na matengenezo ya barabara, madaraja na vivuko.

Pamoja na majukumu hayo Wizara pia inasimamia ukarabati wa majengo ya Serikali, huduma za Ufundi na umeme, kusimamia shughuli za usajili wa Makandarasi, Wahandisi, Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, Usalama barabarani na mazingira katika sekta hiyo.

Pia Wizara inasimamia uboreshaji, utendaji na uendelezaji wa watumishi wa Wizara pamoja na kusimamia utekelezaji wa majukumu ya Wakala,Taasisi na Bodi zilizo chini ya Wizara.

Taarifa hii imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano Serikali
Wizara ya Ujenzi

21/05/2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...