Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MKALI wa muziki wa kizazi kipya, Mbwana Mohamed Mb Dog, amesifia video ya wimbo wake mpya ya Mbona Umenuna akisema imeandaliwa kwa kiwango cha juu na kudhihirisha ubora wake.
Mb Dog 
Akizungumza leo asubuhi jijini Dar es Salaam, Mb Dog alisema mashabiki wote watakaopata bahati ya kuitazama video hiyo iliyotengenezwa na Abby Kazi, ataamini makali yake.
Alisema lengo lake ni kuwapatia mashabiki burudani kamili, hivyo wadau wote wapate muda wa kuitazama video hiyo iliyoachiwa rasmi mwishoni mwa wiki iliyopita, sambamba na kuingizwa kwenye mitandao ya kijamii, youtube na blogs. 
“Hii ni safari yangu ya kurudi katika makali yangu ya zamani, hivyo naamini wimbo wangu ulipokewa kwa shangwe na sasa nimeachia video.
“Mashabiki wote naomba waniunge mkono kwa kuiangalia kazi hii na kusubiri mambo mazuri zaidi kutoka kwangu, maana mipango yangu ni kufanya kazi nzuri zaidi ya Bongo Fleva,” alisema.
 
Katika video hiyo, msanii huyo anaonyesha ujuzi wa aina yake wa kuimba, huku mdundo ‘beat’ yake ikipigwa kisasa zaidi kulingana na mabadiliko ya kisanii kwa wakali wengi Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...