Washiriki wa Miss Tabata 2014 wakiwa kwenye pozi.

Shindano la kumtafuta Redds Miss Tanzania Tabata 2014 limepangwa kufanyika Juni 6 katika ukumbi wa Da’ West Park.

Mratibu wa Miss Tabata Joseph Kapinga alisema kuwa warembo 24 watachuana vikali kutaka kumrithi Dorice Mollel ambaye anashikilia taji hilo.

Dorice pia ndiye anayeshikilia taji la Redds Miss Ilala.

Kapinga alisema kuwa warembo hao wanaendelea kujifua katika ukumbi wa Da’ West kila siku kuanzia saa nane mchana chini ya waalimu wawili, Neema Mchaki na Pasilida Mandali.

Mratibu huyo alisema fainali hiyo itasindikizwa na aina mbali mbali ya burudani ikiwemo wasanii kutoka nje ya nchi.

Warembo wanaendelea na mazoezi kila siku ni Esther Frank Kiwambo (20), Badra S. Karuta (20), Mercy Mathias Kazula (19), Lydia Charles (22),  Nuru Omary Athumani (19) na Happyclarrice Wilson Mbahi (19).

Wenine ni Evodia Peter (22), Fatma Hussein Ismail (20),  Ambasia Lucy Mally (22), Faudhia Hamisi (21), Najma Charles Mareges (19), Lightnes Olomi (18), Husna Ibrahim (19), Ramta Mkadara (20) na Mariam Shwaib Hussein.

Warembo watano kutoka Tabata watashiriki kwenye shindano la kanda ya Ilala, Redds Miss Ilala baadaye mwaka huu.

Miss Tabata inaandaliwa na Keen Arts na Bob Entertainment.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...