Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni inayojumuisha wilaya ya Kinondoni, mkoa wa Pwani (Wilaya ya Kibaha na Bagamoyo) na mkoa wa Tanga Bi Zahra Kayugwa akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa PPF katika viwanja vya Tangamano. Mfuko wa Pensheni wa PPF unawakaribisha Wanachama na Wadau wote kutembelea katika banda lao ili kupata elimu kuhusu mafao na huduma mbali mbali zitolewazo na PPF.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Abdallah Kigoda akisikiliza kwa makini maelezo ya Mfuko wa Pensheni wa PPF kutoka kwa Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni inayojumuisha wilaya ya Kinondoni, mkoa wa Pwani (Wilaya ya Kibaha na Bagamoyo) na mkoa wa Tanga Bi Zahra Kayugwa wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya 2 ya Kibiashara mkoani Tanga.
Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni Bi Zahra Kayugwa akiwa katika picha pamoja na washiriki wengine wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya 2 ya Kibiashara mkoani Tanga katika viwanja vya Tangamano.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...