Na John Gagarini, Kibaha 
CHAMA cha Msalaba Mwekundu mkoani Pwani kimesema kuwa kitaendela kuisaidia jamii ambayo inauhitaji pamoja na wale wanaokumbwa na majanga mbalimbali. 
Hayo yamesemwa  mjini Kibaha na katibu msaidizi wa chama hicho Felisiana Mmasi wakati wakitoa misaada ya viatu na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu na vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu vya THADEI na Buloma vilivyopo kata ya Picha ya Ndege na Mkuza wilayani Kibaha. 
Mmasi alisema kuwa lengo la chama hicho ni kuwasaidia watu wenye matatizo mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni pamoja na kutoa msaada kwenye majanga na maafa yanoyojitokeza. 
 "Mbali ya kutoa viatu pia tumetoa madaftari na kalamu ambapo tutaendelea kusaidia wanafunzi waishio kwenye mazingira magumu kwenye mkoa mzima ambapo baadhi ya wilaya tayari zimeshapatiwa misaada hiyo," alisema Mmasi. 
Kwa upande wake mratibu wa mradi wa Life kupitia chama hicho Kibaha Mjini Agnes Lubogo alisema kuwa mbali ya kusaidia kutoa misaada mbalimbali pia wanasaidia kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI walio majumbani. 
Lubogo alisema kuwa wanahudumia wagonjwa ambao watoro ambao hawapati huduma mahospitalini hivyo kuwafuata huko waliko ambapo wana wahudumu wa nyumbani wapatao 73.

OFISA WA RED CROSS PWANI ISARIA TOWO AKIWAPATIA MADAFTARI
WANAFUNZI WA KITUO CHA THADEI MADAFTARI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA CHAMA HICHO YALIYOFANYIKA MJINI KIBAHA PICHA NA JOHN GAGARINI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...