Kufuatia
wilaya ya Makete mkoani Njombe kuwa miongoni mwa wilaya zenye watoto
yatima, wafanyakazi wa chuo cha VETA Makete wametembelea kituo cha
kulelea watoto yatima cha Bulongwa kilichopo wilayani hapa na kutoa
misaada mbalimbali
Akizungumza
na mwandishi wetu kwa niaba ya wafanyakazi wenzake alioambatana nao Bw.
Mathew Komba amesema wao kama VETA Makete wameguswa na namna watoto hao
wanavyopata tabu kwani hawakupenda kuishi maisha hayo lakini kutokana
na kufiwa na wazazi wao ndiyo maana wapo katika kituo hicho
Amesema
awali walikuwa wamepanga kuwatembelea watoto hao kabla ya pasaka lakini
kutokana na sababu zisizoepukika walishindwa kufanya hivyo lakini
walijipanga kama walivyokuwa wamedhamiria na jana walifika kituoni hapo
kuwaona watoto hao na kuwapa msaada huo
Bw.
Komba amesema baadhi ya vitu walivyovikabidhi ni pamoja na mafuta ya
kupikia, sukari, mchele, sabuni, juisi, dawa za meno na vingine vingi
vyote vikiwa na thamani ya tsh. 329,000/=
Amewaomba
wadau wengine kuwaunga mkono kwa kwenda kuwasaidia watoto yatima kwani
ni jukumu la jamii kwa ujumla kuhakikisha wanawatunza watoto hao licha
ya kwamba wanalelewa kwenye vituo mbalimbali
Kwa
upande wake Bi Sekela Nkyami kutoka kituo hicho cha kulelea watoto
yatima Bulongwa amesema ingawa kituo hicho kina vitega uchumi mbalimbali
lakini bado kinategemea misaada kutoka kwa wafadhili mbalimbali
wakiwemo wakazi wa Makete wenye moyo wa huruma kama walioufanya chuo cha
VETA
Amesema
watoto hao waliopo katika kituo hicho si mali ya kituo pekee bali ni wa
jamii yote kwa hiyo kuiomba jamii kushirikiana nao katika matunzo ili
watoto hao wasijisikie wapweke kutokana na uyatima walio nao
"Ni
kweli uyatima unatesa, ila tunawaomba wananchi waje kutoa misaada
mbalimbali kwa watoto hawa, kumekuwa na kasumba kuwa wakishaletwa hapa
basi si wao tena bali ni wa kituo, hii sia sawa bali tunatakiwa
tushirikiane kwa pamoja chochote kidogo utakachokipata kinatosha
kutusaidia" amesema Bi. Nkyami
Wafanyakazi wa VETA Makete wakiwa katika picha na watoto yatima wa kituo cha Bulongwa.
Mfanyakazi wa VETA Makete akiwa amembeba mtoto yatima anayelelewa kituoni hapo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...